UJIO WA WAMISIONARI WA SHIRIKA LA WAKONSOLATA NA HARAKATI ZA KULETA MAENDELEO HAPA NCHINI; Ujio wa wamisionari wa shirika la Wakonsolata hapa nchini mwishoni mwa karne ya 18, umetoa changamoto kubwa katika nyanja za maendeleo pamoja na kuleta chachu muhimu kwa jamii ya wananchi wa hapa nchini kutokana na wamisionari hao kujikita zaidi katika shughuli za kijamii na kuifanya jamii ya wananchi katika maeno ambayo walifika ambapo mkoa wa Iringa ni mmoja ya sehemu ambazo mabadiliko ya kimaendeleo hayo yamesababishwa na ujio huo. Wamisionari hao wa shirika la wakonsolata waliofika hapa nchini hususani mkoani Iringa, walikuwa ni mapadre, mabruda, masista na walei ambao kwa mara ya kwanza walifika kijiji cha Tosamaganga ambapo walifanya masikani yao na pia wote kwa pamoja walikuwa na lengo la kumkomboa binadamu wa kiafrika wa Tanzania na pamoja na shughuli zingine zote walizofanya za kijamii kiuchumi, kielimu, afya, mawasiliano walizingatia roho yao ya sala na kazi. Ingawaje shughuli zao...