Skip to main content

Posts

Showing posts from September 20, 2015

MAGUFULI ALIVYOITIKISA MJI WA CHATO LEO MKOANI GEITA

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akifafanua jambo kwa msisitizo mkubwa wakati akiwahutubia wakazi wa Chato na vitongoji vyake jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni uliofanyika uwanja wa shule ya sekondari Chato mkoani Geita. Wakazi wa Chato na Vitongoji vyake wakifuatilia na kusikiliza sera za Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akijinadi na kuomba ridhaa mbele yao jioni ya leo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari chato mkoani Geita. Wakazi wa Chato wakishangilia kuonesha kuwa watampa kura za ushindi Mgombea Urais wa CCM Dkt Magufuli kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25 mwaka huu,kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika shule ya sekondari Chato,jioni ya leo mkoani Geita.  Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwahutu...

LOWASSA ATUA BUKOBA KWA KISHINDO...!

Umati wa Wananchi wa Mji wa Bukoba wakionyesha alama ya "Mabadiliko" (change", inayotumiwa na UKAWA, wakati Mgombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitiua CHADEMA, akiwakilisha vuguvugu la Umoja wa Katiba ya Wananchi, Edward Lowassa, alipohutubia maelfu ya watu kwenye mkutano wake wa kampeni uwanja wa Aghakhan mjini Bukoba, mkoani Kagera. Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akihutubia wananchi Bukoba waliofika kwenye Mkutano wa Kampeni, kusikiliza sera zake, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera jana. Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwanadi baadhi ya wagombea wa Udiwani wa vyama vinavyouda UKAWA, kwenye Mkutano wa Kampeni, kusikiliza sera zake, uliofanyika kwenye Uwanja wa AghaKhan, Mjini Bukoba, Mkoani Kagera jana. Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAW...

MABASI YA MWENDO KASI YATUA DAR, KUANZA "KUSANYA" ABIRIA MWEZI OKTOBA

Mabasi ya mwendo kasi, yakishushwa kutoka melini kwenye bandari ya Dar es Salaam, leo Septemba 20, 2015. Mabasi 138 ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) yaliyowasili katika Bandari ya Dar es Salaam, kwa ajili ya kuanza kutoa huduma ya usafiri katika kipindi cha mpito kwenye miundombino ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka (BRT), kuanzaia mwezi Oktoba, 2015, Maafisa wanaosimamia mradi huo wamewaambia waandishi wa habari kagtika hafla ya kuyapokea mabasi hayo iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick na viongozi wa DART Mkuu wa Mkowa Dar es Salaam, Bw. Saidi Meck Sadiki (kulia) akiwa katika bandari ya Dar es Salaam alipofanya ziara ya kujionea kuwasili kwa Mabasi 138 ya Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) tayari kuanza kwa kuanzahuduma ya kipindi cha mpito mwezi ujao,kushoto ni Kaimu Meneja Bandari ya Dar es Salaam, Bw.Hebel Mhanga, wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni UDA Rapid Transit (UDA-RT), Robert Kisena ambaye pia ni Mwekiti wa Kampuni ...

MGOMBEA UDIWANI KATA YA MBAGALA KUU (CCM) YUSUF MANJI AZINDUA KAMPENI ZAKE

Kiongozi wa Kamati ya Ushindi kwa CCM kutoka Kigoma, Nicholaus Zacharia (kulia), akimtambulisha Yusuf Manji katika uzinduzi huo. Mgombea nafasi ya udiwani Kata ya Mbagala Kuu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Manji (kushoto), akihutubia wananchi na makada wa chama hicho katika uzinduzi wa kampeni uliofanyika eneo la Kichemuchemu Kaskazini Dar es Salaam leo jioni. Kiongozi wa Kamati ya Ushindi kwa CCM kutoka Kigoma, Nicholaus Zacharia, akihutubia katika uzinduzi huo. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Wilaya ya Temeke, Sophia Kinega akihutubia kwenye uzinduzi huo. Mchumi wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Neema Urio akihutubia kwenye uzinduzi huo. Kada wa CCM, Godbertha Kinyondo akisalimia wananchi kwenye uzinduzi huo. Makada wa CCM wakiserebuka Vijana wa hamasa wa CCM wakiwa kazini. Wananchi wakiwa kwenye mkutano huo. Michango mbalimbali ikitolewa. Umati ukimsikiliza Yusuf Manji. Mkazi wa eneo hilo, Sharifa Ali akimueleza Manji ku...