Skip to main content

Posts

Showing posts from November 5, 2013

SHULE YA PERAMIHO INAONGOZA KIWILAYA

  Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Peramiho, Jane Mkuwa. (Picha na Friday Simbaya) Na Friday Simbaya, Songea Shule ya Msingi Peramiho, Wilaya  Songea Vijijini mkoani Ruvuma,  imepanda na kushika nafasi ya kwanza kiwilaya kutoka nafasi ya pili mwaka jana kati ya  ya shule 89, imefahamika. Akiongea  na MWENGE, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Peramiho,  Jane Mkuwa leo ofisini kwake alisema shule yake imepanda nafasi ya kwanza kiwilaya kati ya shule 89 ukilinganisha na mwaka jana ambapo shule hiyo ilishika nafasi ya pili. Aidha, shule hiyo imekuwa  ya sita kimkoa kati ya shule 719 na nafasi ya 428 kitaifa kati ya jumla ya shule 15,656. Shule hiyo  ina jumla ya walimu 20 wakiwemo  walimu wa kike  kumi na tano na wakiume wa  tano. Alisema kuwa watahiniwa waliofanya  mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa mwaka 2013  walikuwa 33 na wote  wamefaulu, sawa na asilimia 100 ya ufaulu. Wanafunzi waliopata alama za juu kulik...