Skip to main content

Posts

Showing posts from September 30, 2011

NGURUWE 612 WAFA KWA MAFUA LUDEWA DC APIGA MARUFUKU WATU KUMLA MNYAMA HUYO

LUDEWA MKUU wa Wilaya ya Ludewa Bi. Georgina Bundala amepiga marufuku kwa muda usiojulikana kuchinja au kula na kusafirisha nguruwe pamoja na mazao yake kama vile nyama, mifupa, nywele na mazao ya kusindika kutokana na homa ya nguruwe kupiga hodi tena wilayani humo. Bi. Bundala alisema endapo mfanyabiashara au mfugaji yeyote atabainika akisafirisha nguruwe kutoka katika maeneo yaliyoathirika na kupeleka maeneo yasiyoathirika mtu huyo atakuwa amekiuka agizo na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake. Aidha amewaagiza wataalamu wote wa kilimo na mifugo, maafisa watendaji kata na vijiji kusimamia agizo hili ili kuwathibiti wale wote wasiokuwa waaminifu wanaosafirisha nyama ya nguruwe kwa siri wakidhani wanajificha. Akitoa taarifa na takwimu za ugonjwa huo kwa Mkuu wa Wilaya, Daktari wa Mifugo wilayani Ludewa Bw. Festo Mkomba alisema maambukizi mapya ya homa ya nguruwe yametokea katika tarafa ya Mwambao wa Ziwa Nyasa na sasa yapo katika tarafa ya...

WAHASIBU KORTINI KWA WIZI WA MILIONI 79.8 MAKETE

Makete WATUMISHI wanne wa Halmashauri ya wilaya ya Makete kitengo cha fedha wamefikishwa mahakamani kwa makosa 233 yakiwemo wizi wa fedha zaidi ya 79.8m/- mali ya umma. Watumishi hao ni pamoja na Bw. Golden Asheri Sanga Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu katika Halmashauri hiyo na mke wake aitwaye Bi. Naheri Paten Chengula ambaye ni mwalimu katika Shule ya Msingi Makete. Wengine waliofikishwa mahakamani hapo ni pamoja na Sued Abdul Milanzi na Ernest Mwangomela wote wahasibu wasaidizi katika halmashauri hiyo ya Makete. Akisoma hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo mheshimiwa Chanjalika mwendesha mashtaka mrakibu msaidizi wa polisi ambaye ni mkuu wa upelelezi wilaya ya Makete ASP Komba aliiambia mahakama kuwa washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 233 ikiwemo wizi. Bw Komba aliyataja makosa mengine kuwa ni pamoja na wizi wakiwa watumishi, kula njama za kuiibia serikali na kuingiza hesabu za uongo katika vitabu ...