Iringa. Mwenyekiti wa Wazazi Wenye Watoto Wenye Ulemavu Mkoa wa Iringa, Bw. Zawadi Msigalla, amesema ana ndoto ya siku moja kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuwatetea watu wenye ulemavu na makundi maalum, akimuomba Rais Samia Suluhu Hassan amkumbuke katika nafasi 10 za uteuzi wa wabunge. Bw. Msigalla, ambaye ni mtu mwenye ulemavu, amesema dhamira yake ya kuingia bungeni inatokana na uzoefu wake wa muda mrefu katika utetezi wa haki za watoto wenye ulemavu na wazazi wao, akibainisha kuwa sauti ya kundi hilo bado haijapewa uzito unaostahili katika vyombo vya maamuzi. “Nina ndoto ya kuwa Mbunge ili niweze kuzungumza kwa niaba ya wazazi na watoto wenye ulemavu. Tuna changamoto nyingi zinazohitaji uwakilishi wa moja kwa moja,” amesema Msigalla. Akizungumza na Pamlomo- Sauti Ya Jamii mesema anaamini kuwa kupitia nafasi za uteuzi wa Rais, bado kuna fursa kwa watu wenye ulemavu na watetezi wao kushiriki kikamilifu katika kutunga na kusimamia sheria. Mbali na kuwa mwenyekiti w...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.