Skip to main content

Posts

Showing posts from March 26, 2017

MAGAZETI YA LEO JUMATATU

MANISPAA YA IRINGA YATOA MKOPO WA 70M/- KWA WANAWAKE NA VIJANA

HALMASHAURI ya Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa imetoa mkopo kwa vikundi 35 vya wanawake na vijana ikiwa ni utekeleza wa agizo la serikali la kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi hivyo jana. Akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 70,000,000/- kwa vikundi hivyo katika awamu ya pili ya kipindi cha mwaka 2016/2017, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Alex Kimbe amewataka kinamama na vijana kutumia fedha hizo kwa shughuli zilizokusudiwa ili ziweze kuleta manufaa na kuwatoa katika lindi la umasikini. Alisema kuwa jumla ya vikundi 35 toka katika kata zote 18 za Manispaa ya Iringa vimepokea mikopo, ambapo vikundi 16 vya vijana vimepokea jumla ya shilingi milioni 32,000,000/- na shilingi milioni 38,000,000/- zimetolewa kwa vikundi 19 vya wanawake. Kimbe alisema mkopo huo umetolewa kwa awamu ya pili, ambapo kwa awamu ya kwanza kipindi cha mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Manispaa ya Iringa i...

ZAIDI YA 80 IRINGA WAPATA MAFUNZO YA UKARIMU NA UTALII

Mwenyekiti wa vikundi vya asili vya ngoma kutoka Ikwavila New Force katika Kijiji cha Mahuninga, tarafa ya Idodi wilayani Iringa, mkoani Iringa, Recktika Palinoo (wa mbele kulia) pamoja na katibu wake Leonatus Kikoti wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya siku tatu ya ukarimu na utalii yaliyofanyika mkoani Iringa jana.   (Picha na Friday Simbaya) MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka watoa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii kanda ya kusini kuboresha huduma zao ili kukidhi haja soko la utalii katika ukanda huu. Alisema kuwa ili kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za taifa za kusini watoa huduma kwa kushirikiana na sekta binafsi hawanabudi kuinua viwango vya utowaji wa huduma. Masenza alisema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watoa huduma katika sekta ya ukarimu na utalii yaliyofanyika mkoani Iringa jana. Alisema kuwa serikali ipo katika machakato wa kuboresh...

MANISPAA YA IRINGA YAAGIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA ZINGATIA VIWANGO VYA UBORA

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)imeiagiza Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa kuboresha barabara zake za pembezoni mwa mji ili zitoe huduma kwa wananchi. Akizungumza wakati wa majumwisho wa ziara ya siku moja ya kamati kwenye Manispaa ya Iringa jana makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Abdallah Chikota alitoa maelekezo kuboresha miundombinu ya barabara pembezoni mwa mji. Alisema kuwa Manispaa ya Iringa imeelekeza nguvu kubwa katikati ya mji na kusahau barabara za pembezo ambazo zitasaidai kutoa huduma kwa wananchi. Chikota alisema kuwa wananchi walioko pembezoni mwa mji ni sawa na wananchi wa katikati ya mji. Kuna tofauti kubwa kati ya wananchi waishio pembezoni na katikakti. Barabara za pembezoni mwa mji hazina kiwamgo vya ubora…,” alisema Chikota. Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge za Hesabu za Serikali za Mitaa ilitembelea barabara za Mkimbizi- kihesa Sokoni-Tumaini Univesrsity and Ngome na kukuta havian vivuko kwa kurahisha ...