Skip to main content

Posts

Showing posts from February 15, 2026

Abanywani Watinga Iringa kwa Shangwe: Wahaya Waaga 2025, Wakumbatia 2026 kwa Kishindo

Iringa. Jamii ya Wahaya wanaoishi Manispaa ya Iringa imefanya sherehe maalumu ya kuuaga mwaka 2025 na kuukaribisha mwaka 2026 kwa shamrashamra kubwa, katika hafla iliyopewa jina la “Abanywani” likimaanisha marafiki. Sherehe hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Iringa iliwakutanisha Wahaya kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa huo wakiwemo familia, vijana na wazee, kwa lengo la kuimarisha mshikamano, kuendeleza utamaduni wao na kusherehekea mafanikio ya mwaka uliopita. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, mmoja wa waandaaji Kaijage Rwezaula alisema neno Abanywani linaakisi urafiki, upendo na umoja miongoni mwa wanajamii, huku likiwaalika pia watu wa makabila mengine kushiriki na kujifunza utamaduni wa Kihaya. “Tumekutana hapa si tu kwa ajili ya burudani, bali kuimarisha undugu wetu na kusaidiana kama marafiki na ndugu tunaoishi mbali na nyumbani,” alisema Kaijage Katika sherehe hiyo, washiriki walipata fursa ya kufurahia vyakula vya asili ya Kihaya, muziki wa asili pamoja na bur...

NIGERIA YAONGOZA VIWANGO VYA WANAWAKE AFRIKA KWA MUJIBU WA FIFA

Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, limetangaza viwango vipya vya timu za taifa za wanawake barani Afrika (CAF), huku Nigeria ikiendelea kushika nafasi ya kwanza kwa ubora wa soka la wanawake barani humo. Kwa mujibu wa orodha hiyo ya viwango vya wanawake Afrika chini ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Nigeria inaongoza, ikifuatiwa na South Africa katika nafasi ya pili, huku Morocco ikishika nafasi ya tatu. Katika nafasi ya nne ni Ghana, wakati Cameroon ikishika nafasi ya tano. Zambia ipo katika nafasi ya sita, ikionesha kuimarika kwa soka la wanawake katika ukanda wa kusini mwa Afrika. Orodha hiyo pia inaonesha Ivory Coast katika nafasi ya saba, ikifuatiwa na Tunisia katika nafasi ya nane. Mali ipo nafasi ya tisa, huku Equatorial Guinea ikifunga kumi bora. Nigeria imeendelea kuwa kinara wa soka la wanawake Afrika kutokana na historia yake ya kutwaa mataji mengi ya bara hilo na kushiriki mara kwa mara katika michuano ya Kombe la Dunia la Wanawake. Hata hivyo, ushindani umeongezek...