Skip to main content

Posts

Showing posts from October 19, 2015

UNDP YASISITIZA VITA YA UMASKINI KWA KUTUMIA MAZINGIRA

Mkurugenzi Msaidizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) Tanzania, (Ushauri na Miradi), Amon Manyama akitoa maelezo kuhusu mradi wa PEI na salamu kutoka UNDP kwa washiriki wa mafunzo hayo hivi karibuni jijini Mwanza. Na Mwandishi Wetu, Mwanza MKURUGENZI Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Amon Manyama, alisema vita dhidi ya umaskini inakuwa na maana kubwa kama inalinganishwa na mazingira. Alisema kwamba umaskini wa kipato ambao umekuwa ukipiganwa sana kwa sasa unastahili kupiganwa kwa kuangalia umaskini kutokana na ukweli kuwa kuboreshwa kwa mazingira ndio hatua kubwa ya kupigana na umaskini katika sura zote zilizobaki. Mkurugenzi msaidizi huyo alisema hayo hivi karibuni mjini Mwanza wakati akielezea mradi wa mtaji na elimu wa UNDP ambao umefanyiwa kazi kwa pamoja kati ya shirika hilo, Tume ya Mipango, Hazina na Ofisi ya Makamu wa Rais, katika mafunzo ya siku moja ya Uimarishaji wa Ushirika wa Akiba na Mikopo, yaliyofanyika ...

UN, SMZ KUSHIRIKIANA KUKOMESHA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto, Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Kijiji cha Mahonda wakati wa ziara fupi ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa visiwani humo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja huo tangu kuanzishwa. Na Mwandishi wetu, Zanzibar. Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez amesema Umoja huo utaendelea kushirikiana na Serikali ya mapinduzi Zanzibar (SMZ) katika kukomesha vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia. Akizungumza katika ziara ya kutembelea Dawati la jinsia la Wanawake na Watoto, Mkoa wa Kaskazini Unguja katika Kijiji cha Mahonda alisema umoja huo umelenga kusaidia uwepo wa utawala wa sheria na wenye kujali haki na utu wa binadamu kupitia mpango mkakati wake uliomo katika malengo ya m...

MAGZAETI LEO JUMANNE

MKUTANO WA TUME NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA...!

Kamishna wa tume ya uchaguzi ya taifa Jaji (Mst) Mary Longway (katikati) akitoa hotuba wakati wa mkutano wa tume na viongozi wa vyama vya siasa leo mjini Iringa. Mkutano huo ulikuwa wa kujadiliana na kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ya uchaguzi na pia kupeana taarifa kuhusu maandalizi ya Uchaguzi Mkuu hapo tarehe 25 Oktoba 2015. Kutoka kushoto walioketi ni Afisa wa tume ya uchaguzi ya taifa William Kitebi na mratibu wa uchaguzi mkoa wa iringa, Wilfred Muyuyu. Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Iringa Mustafa Msovela akiuliza swali tume kuhusu mgongano wa matamko kati ya viongozi wa siasa na tume juu ya kusimama mita 200 kutoka kituo cha kupigia kura pamoja na kulinda kura baada ya kupiga kura wakati wa mkutano wa tume na viongozi wa vyama vya siasa leo mjini Iringa.  Katibu Mkuu wa CHAUSTA -Taifa Mwaka Lameck Mgimwa akiuliza swali kuhusu utata wa wanavyuo kupiga kura ya urais pamoja na wale waliohama baada ya zoezi la uhakiki la dafatri la wapiga...