Skip to main content

Posts

Showing posts from February 17, 2016

WAZIRI WA AFYA MH. UMMY MWALIMU NA NAIBU WAKE WATEMBELEA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI KUKAGUA

Tazama video ya tukio hilo hapa : Dk.Stanslaus Ntiyakunze (aliyenyoosha mkono) akiwaonyesha mawaziri namna jengo linavyokarabatiwa ikiwemo miundombinu yake inavyotakiwa kuwa pindi litakapokamilika ikiwemo suala la mfumo wa maji safi na maji taka. Kuliwa kwake ni Naibu Waziri wa Afya Dk Hamisi Kigwangalla wengine Kaimu Mkurugenzi wa hospitali hiyo ya Muhimbili, Prof. Laurance Masaru (kushoto) na Waziri wa Afya, Mh. Ummy Mwalimu (katikati). Mawaziri wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli wameendelea kufanya kile ambacho wananchi wanataka ikiwemo suala la kutumikia wananchi ambapo mapema leo, Februari 17, Mawaziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu na Naibu wake, Dk. Hamisi Kigwangalla wameweza kutembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa lengo la kukagua majengo likiwemo lile aliloagiza Rais kuwa litumike kuwa wodi ya akina mama. Mawaziri hao wamefika Hospitali hiyo ya Taifa majira ya mchana na kisha kupokel...

Wateja wa Tigo, AzamTV na LigaBBVA kwenda kuangalia mechi ya Barcelona bure

Mtendaji Mkuu wa Azam TV, Rhys Torrington (kushoto) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Promosheni ya kujishindia safari ya kwenda kushuhudiamechi ya Ligi Kuu ya Hispania maarufu kama La Liga, kati ya Deportivo la Coruna na Barcelona Machi mwaka huu . Katikati yake ni Meneja Promosheni wa Tigo Pesa, Mary Rutta.Kulia kwake Mkuu wa Idara ya Masoko ya Azam TV, Mgope Kiwanga .Promosheni hiyo ya ushirikiano wa Tigo Pesa na Azam TV, inaanza rasmi leo hadi Machi 13 na washindi wawili watakwenda Hispania. Tigo, Azam Media na LigaBBVA leo wametangaza  ushirikiano baina yao ambao utawapa fursa watumiaji wa huduma Tigo Pesa wanaonunua vifurushi vya michezo vya AzamTV  kupata nafasi ya kusafiri bure bila malipo kwenda kutazama mechi ya ligi kuu  kati ya miamba wawili wa Hispania – Barcelon na Deportivo la Coruna – itakayofanyika Aprili mwaka huu. Akiongea katika uzinduzi wa promosheni hiyo leo jijini Dar es Salaam,  Meneja wa Promosheni wa Tigo Pesa, ...

TAASISI YA TANZANIA WOMEN OF ACHIEVEMENT (TWA) YAZINDUA KAMPENI YA UWIANO WA KIJINSIA

Rais wa Taasisi ya TANZANIA WOMEN OF ACHIEVEMENT (TWA) (TWA), Irene Kiwia (katikati ) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani ) kuhusu uzinduzi wa kampeni ya uwiano wa kijinsia ambayo ni kauli mbiu kuelekea kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani, kushoto kwake ni Balozi wa kampeni ya uwiano sawa kijinsia Inspk.Prisca Komba na kulia kwake ni Mwenyekiti wa TWA, Sadaka Gandi kwenye mkutano uliofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.  Mwenyekiti wa Taasisi ya TANZANIA WOMEN OF ACHIEVEMENT (TWA), Sadaka Gandi akifafanua jambo kuhusu uzinduzi wa kampeni ya usawa wa kijinsia kwenye mkutano na waaandishi wa habari uliofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.  Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakisikiliza kwa makini maelezo kutoka kwa Rais wa TWA Irene Kiwia kuhusu uzinduzi wa kampeni ya usawa wa kijinsia katika mkutano uliofanyika mapema leo Jijini Dar es salaam . Dar es Salaam, Februari 17, 2016: Taas...

DK. KIGWANGALLA AUPA MIEZI SITA UONGOZI WA HOSPITALI YA RUFAA MOROGORO KUREKEBISHA MFUMO WA CHUMBA CHA UPASUAJI

Dk. Kigwangalla akimsikiliza mtoa huduma kwa njia ya mtandao katika malipo (hayupo pichani) alipotembelea hospitalini hapo. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro mapema jana Februari 16 na kubaini matatizo mbalimbali ikiwemo chumba cha upasuaji, mfumo wa malipo na ubovu wa vifaa vya maabara. Dk. Kigwangalla ametoa siku 60 vifaa ndani ya chumba cha upasuaji ziwe zimerekebishwa huku akiagiza ndani ya miezi sita mfumo wa chumba cha upasuaji uwe umetengenezwa vizuri na endapo watashindwa basi atachukua hatua za kufungia vyumba hivyo vya upasuaji kwani vikiendelea kuachwa hivyo vitaendelea kusababisha matatizo Zaidi kwa wanaopaatiwa huduma. Dk. Kigwangalla akiwa ameambatana na Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk. Ritha Lyamuya walitembelea vitengo kadhaa ikiwemo chumba cha upasuaji, jengo la maabara, pamoja na majengo mengine ikiwemo lile la wamam...

REGIONAL WORKSHOP ON MAKING AN IMPACT WITH HUMAN DEVELOPMENT REPORTING STARTS

The host of the workshop, Executive Director of ESRF, Dr. Tausi Kida, presents a paper; The Tanzania human development report experience. The session highlighted the Tanzania report experience in producing the Tanzania human development report 2014/2017. UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, delivers his speech when opening a four-day regional workshop on making an impact with human development reporting at Ramada Resort in Dar es Salaam, February 16, 2016. Executive Director of Economic and Social Research Foundation, ESRF, Dr.Tausi Kida congratulates the UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania, Mr.Alvaro Rodriguez, after he had delivered his opening remarks. Rodgers Dhliwayo, Economics Adviser/Senior Economist UNDP Tanzania Country Office, presents a paper; Influence of the National Human Development Reports (NHDRs)-Why Produce NHDRs?, during the morning session of four-day regional work...

MWENYEKITI WA BODABODA MKOANI MWANZA ATOA TAHADHARI JUU YA VITENDO VYA UKWAPUAJI JIJINI MWANZA

Mwenyekiti  wa Chama cha Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda (pichani), amewataharisha wakazi wa Jiji la Mwanza kuwa makini wawapo barabarani, ili kuepukana na  vitendo vya ukwapuaji wa Mikoba na Mabegi vinavyofanywa na baadhi ya wahalifu  kwa kutumia pikipiki. Kayanda alitoa tahadhari hiyo jana Jijini Mwanza baada ya kupokea  malalamiko ya kukithiri kwa vitendo vya ukwapuaji vinavyofanywa na baadhi ya  watu wanaojifanya waendesha pikipiki, jambo linalochafua taswira ya waendesha  pikipiki Mkoani Mwanza. Tayari watu kadha wamefikisha malalamiko yao kwa uongozi wa bodaboda Mkoani Mwanza, baada ya kukumbwa na  kadhia ya kukwapuliwa mikoba pamoja na mabegi yao, ambapo mmoja wa wahanga wa  matukio hayo Diana Abdallah ameeleza kukwapuliwa mkoba wake uliokuwa na pesa  pamoja na vito vya thamani wakati akitokwa kwenye shughuli zake. "Nilikuwa maeneo ya Nyegezi ambapo nilikuwa nikitoka kwenye shughuli zangu, nilikwap...

WANACHACHAMA WA CCM MKOANI MWANZA WAONYA VITEGA UCHUMI VYA CHAMA KUTUMIKA VIBAYA

Wanachama wa  Chama cha Mapinduzi CCM, Kata ya Kirumba Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza,  wameonya juu ya baadhi ya Wawekezaji nchini wanaotumia Vitega uchumi vya chama  hicho bila kufuata mikataba wanayopewa. Wanachama hao walitoa kauli hiyo wiki hii baada ya Wawekezaji wanaotumia majengo ya CCM Kata ya Kirumba, kudaiwa kukiuka masharti yao na  hivyo kutumia majengo hayo bila kuyalipia kodi ya pango kwa muda mrefu. Ni kutokana na hatua hiyo, Wanachama hao walichukua maamuzi ya  kufunga Majengo hayo ambayo yanatumiwa na Tasisi ya Mikopo ya Wadoki pamoja na  Hotel ya Kirumba Resort, huku taratibu nyingine za kisheria zikiendelea, lengo  likiwa ni kuhakikisha kwamba watumiaji wa majengo hayo wanayalipia kodivwanayodaiwa  vinginevyo watafurushwa nje ya majengo hayo. Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kirumba Abubakary Francis  Kweyamba alithibitisha kwamba wanachama hao wamefikia maamuzi hayo, kutokana na  kutumia majengo ya c...

PUMBAZUKA NA SIMBAAYA BLOG MAGAZETI YA LEO ALHAMISI