Skip to main content

Posts

Showing posts from March 1, 2013

MAJIMAJI SPORTS CLUB YAPIGWA JEKI

Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Peramiho, Dkt. Venance Mushi katika viunga vya hospitali hiyo jana muda mfupi baada ya hafla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni mbili kwa Timu ya Majimaji kuiwezesha timu hiyo kufika malengo yake.

TIMU YA MAJIMAJI YAPIGWA JEKI

HOSPITALI ya Peramiho, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma imetoa hundi ya shilingi milioni mbili kwa timu ya mpira ya Majimaji (Majimaji Sports Club) jana kwa lengo ya kuisaidia timu hiyo kufikia malengo yake ya kutafuta nafasi ya kucheza Ligi Kuu Bara mwakani. Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dkt. Venance Mushi alisema kuwa hospitali yake kama sehemu kubwa ya jamii ya mkoa Ruvuma na mdau pia wa kuendeleza michezo yote, wameamua kuisaidia timu ya Majaimaji kiasi kidogo pesa, kwa lengo kuiwezasha timu hiyo kufanya vizuri mashindano ya ligi daraja la kwanza yanayoendelea hivi sasa iliweze kusonga mbele. Alisema kuwa Peramiho ikiwa ni sehemu kubwa ya Mkoa wa Ruvuma hawanabudi kuisaidia timu yoyote ile kupanga ushindi na hatimaye kufikia malengo yake.  Aidha, alisema kuwa Hospitali ya Peramiho imeamua kutoa msaada ya shilingi milioni mbili kwa timu ya mpira ya Majimaji ya ilikuwawezesha kutimishiza malengo yake pamoja na kutatua baadhi matatizo timu hiyo. “ H...