Skip to main content

Posts

Showing posts from January 28, 2014

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA INA JUMLA YA WANAFUNZI 3770 WASIOJUA KUSOMA, KUANDIKA NA KUHESABU

Na Friday Simbaya, Songea Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma katika Idara ya Elimu ya Msingi   ina jumla ya wanafunzi 3770 wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu (K.K.K.), imefahamika. Hayo yalibainika wakati   wa mkutano wa kutathmini elimu na matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na daras la nne mwaka 2013 uliofanyika hapa Peramiho hivi karibuni . Akisoma taarifa yake ya utekelezaji kwa wadau wa elimu mbalimbali waliohudhuria kikao hicho cha siku moja, Afisa Elimu Taaluma, Wilaya ya Songea, Vincent Chimoto alisema kuwa wapo wanafunzi wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu katika shule za msingi mwaka 2013 wapatao 3770 darasa la I-VII. Afisa huyo wa elimu taaluma pia aliwaagiza walimu kuchukuwa jitihada za makusudi kwa kutenga muda wa ziada na kuwa na ratiba ya kuwafundisha wanafunzi hao ili wajue stadi za K.K.K. Aidha, alisema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea inazo jumla ya shule za msingi 96, kati ya hizo shule zenye darasa la sa...