Skip to main content

Posts

Showing posts from August 15, 2010

KITIMUTIMU JIMBO LA IRINGA MJINI

BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mjini Iringa katika Jimbo la Iringa Mjini, kesho wameahidi kuanza kurudisha kadi za chama hicho katika ofisi za matwi yao ikiwa ni matokeo ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kumuengua katika kinyang’anyiro cha ubunge, Fredrick Mwakalebela aliyeshinda kura za maoni za chama hicho katika jimbo la Iringa Mjini. Katika kura hizo, Mwakalebela alimshinda kwa kura 3, 897 na mpinzani wake wa karibu Bi.Monica Mbega aliyepata kura 2,989. NEC imemuengua Mwakalebela katika mbio hizo za kuusaka ubunge katika jimbo hilo kumeelezwa kuhusishwa na kashfa ya rushwa inayomkabili. Baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa baadhi ya wanachama walioapa kurudisha kadi za chama hicho na kumuunga mkono mgombea wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), mwandishi wa habari hii jana alitembelea baadhi ya matawi ya chama hicho mjini hapa na kushuhudia makundi ya wanaCCM wakijipanga na kuendelea kuwashawishi wenzao kesho kuziru...

…VIGOGO………….1

ALIYEKUWA mshindi wa pili katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Njombe Kaskazini, Alatanga Nyagawa huenda akatimkia CHADEMA ikiwa ni hatua mojawapo ya kupinga maamuzi ya vikao vya juu vya chama hicho yaliyomteua Deo Sanga (Jah People) kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo. Katika kura hizo, Jah people alipata kura 6,313 dhidi ya kura 2,313 alizopata Nyagawa huku mbunge mkongwe aliyemaliza muda wake Jackson Makweta akipata kura 1,671. Akizungumza kwa njia ya simu jana, Nyagawa alisema yeye pamoja na wanaCCM wengine 11 waliokuwa wakiwania kushinda kura za maoni za jimbo hilo, walipinga matokeo yaliyompa ushindi Jah People kwa madai kwamba yalitawaliwa na mazingira ya hila na rushwa. Nyagawa alisema tofauti na matarajio yake vikao vya juu vya CCM vimetupilia malalamiko yao ambayo yana ushahidi wa kutosha. Nyagawa alisema kutokana na kasoro hizo hayuko tayari kuunga mkono ushindi na uteuzi wa Jah People kuwania ubunge katika jimbo h...

UBALOZI WA UNITED ARAB EMIRATES NCHINI WATOA MSAADA KWA WAISLAM

UBALOZI wa United Arab Emirates (UAE) nchini kupitia kwa Balozi wake Maala llah Mubarak Suweid umetoa msaada kwa waislamu kupitia taasisi ya Dhi nureyn Islamic Foundation yenye makao yake makuu – mkoani Iringa. Msaada huo ambao umetolewa na taasisi mbili za nchini UAE ambazo ni : Sheikh Khalifa Bin Zaid Al Nahyan Foundation for humanitarian aid na Red Crescent Society of UAE , misaada hiyo ni kwa jili ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ambao waislamu hufunga na kuzidisha kufanya mema kwa ajili ya kujikurubisha kwa mwenyezimungu. Akizungumzia kuhusu msaada huo, Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi ya Dhi Nureyn Sheikh Said Ahmed Abri, amemshukuru balozi Maala llah na ubalozi mzima wa UAE kwa msaada huo, na amemuomba afikishe salamu na shukrani za waislamu kwa uongozi mzima wa uae na watu wake. Msaada uliotolewa unafikia shilingi milioni hamsini (50,000,000) ambazo ni : 35,000,000 fedha taslimu kwa ajili ya programu za ufuturishaji na bosks 500 za tende zenye jumla ya kg 6,000 zenye thamani y...