Mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Luckness Amlima Leo ameamuru mbolea iliyokuwa imeletwa wilayani humo kwa ajili ya wakulima wa zao la Tumbaku na madereva kuzuia kushusha mbolea hiyo wakidai walipwe gharama za usafirishaji wa mbolea hizo ameamuru zishushwe mara moja na wagawiwe wakulima. Akiongea na madereva na wakulima hao katika viwanja vya ushirika wilayani humo mkuu wa wilaya huyo alisema kuwa hakuna sababu ya kuendelea kubaki na mbolea kwenye magari huku wakulima wakilalamikia tumbaku inaharibika kwa kukosa mbolea. “Shusheni mbolea kwani madai ya fedha ya kusafirishia mbolea hiyo yanafanyiwa kazi na chama kikuu cha Ushirika SONAMCU alisema mkuu wa wilaya huyo. Aidha mwandishi msaidizi wa chama cha msingi Namtumbo bwana Nasoro Makomaye alisema kuwa mbolea ilifika wiki mbili zilizopita lakini madereva walikataa kushusha mbolea hiyo wakidai fedha ya kusafirishia mbolea hiyo. Bwana Nasoro alimshukuru mkuu wa wilaya ya Namtumbo kwa kuwasi...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.