Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Eng. Stella Manyanya akisalimiana na wanafunzi wa shule za msingi za Mwaya na Tumaini zilizopo kata ya Nyalumbu wilayani Kilolo, mkoani Iringa wakati ya ziara ya ufuatilialiaji wa vituo vya elimu nje ya mfumo rasmi, vituo sitiri na elimu ya watu wazima juzi. (Picha na Friday Simbaya) NAIBU wa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Eng. Stella Manyanya amesikitishwa na kiwango cha hali ya kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu (illiteracy rate) katika Mkoa wa Iringa, ambayo ni asilimia 18. Mkoa wa Iringa una jumla ya watu 941,238 kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012. Eng. Manyanya aliyasema hayo juzi wakati ya ziara yake ya ufuatilialiaji wa vituo vya elimu nje ya mfumo rasmi, vituo sitiri na elimu ya watu wazima, mkoani Iringa. Alisema kuwa takwimu hizo za kuongezeka watu wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu zinahitaji juhudi za serikali ili kufikia malengo ya kimataifa. Alisema ...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.