Skip to main content

Posts

Showing posts from October 19, 2016

ZAIDI YA WADAU 100 UKANDA WA KUSINI WATASHIRIKI MAADHISHO YA UTALII

Ofisi ya mkuu wa mkoa wa iringa kwa kushirikiana na wizara ya maliasili na utalii, mradi wa kuboreha mtandao wa hifadhi zakusini mwa Tanzania (SPANEST) pamoja na na wadau mbalimbali imeazimia kufanya sherehe za maadhimisho ya utalii ukanda wa kusini mwa Tanzania ujulikanao kama ‘karibu Tanzania southern circuit’. sherehe za maadhimisho ya utalii ukanda wa kusini mwa Tanzania unaojumwisha mikoa ya iringa, mbeya, katavi, songwe, morogoro na ruvuma zitafanyika kabla ya tarehe 30 November mwaka 2016 ili kwenda sambamba na maadhimisho yanayofanyika duniani kote. Lengo kuu ya sherehe ya maadhisho hayo ni kukuza na kuendeleza utalii kikanda na taifa kwa ujumla.  Maadhimisho ya Utalii yafanyike kwa Siku 3 kuanzia tarehe 27-29 Novemba, 2016. Tarehe hizo zimechaguliwa ili:- -Kutoa fursa ya kutosha kwa Mkoa kufanya maandalizi ya kufanikisha sherehe hizo. -Kutoa fursa kwa wadau wa Mikoa ya kusini kushiriki katika maandalizi na maonyesho haya ambayo yanafanyika kwa m...

BASI LA KAMPUNI YA BARCELONA LAUA

Watu 10 wamefariki dunia na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Barcelona walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es Salaam kwenda mkoani Lindi kupata ajali eneo na Miteja mkoani Lindi. Taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga imesema kuwa chanzo cha ajali hiyo kimetokana na tairi ya gari ya upande wa kushoto kupasuka na kutokana na mwendo wa kasi wa basi hilo, dereva alipoteza uelekeo ndipo likapinduka. Pia Kamanda Mzinga amesema kuwa wamechunguza na kugundua kua licha ya kuwa basi hilo lilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 48, wakati basi hilo linapata ajali kulikuwa na abiria 54 kitu ambacho ni kosa kisheria. Aidha, Kamanda Mzinga amesema kuwa bado wanaendelea na uchunguzi kuweza kubaini alipo dereva ili kuweza kufahamu ni kipi hasa kilichotokea. Hadi sasa wanamshikilia kondakta wa basi hilo lakini bado hajaweza kuelezea tukio halisi.