Skip to main content

Posts

Showing posts from February 1, 2016

WAHAMIAJI HARAMU 83 WA KIETHIOPIA , DEREVA NA TINGO KUTUPWA JELA MIAKA 3 !

18:48    No comments   MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa imewahukumu kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya Sh Milioni 1.5 kila mmoja, dereva Hansi Mwakyoma (28) na tingo wake wake Alex Adam (32) baada ya kukamatwa na kukiri kusafirisha wahamiaji wasio na vibali 83 kutoka nchini Ethiopia ambao pia wamehukumiwa kwenda jela miaka 3 au kulipa faini ya Sh Milioni 1. Kwa kutumia gari aina ya Scania lenye namba T478 DFE mali ya Frola Mwambenja wa Mbeya, Januari 16, mwaka huu; dereva huyo na tingo wake walikamatwa katika kijiji cha Ruaha Mbuyuni wilayani Kilolo mkoani Iringa, barabara kuu ya Iringa Mbeya wakiwasafirisha watu hao kuelekea Kyela ambako ni mpakani mwa Tanzania na Malawi. Akitoa hukumu hiyo leo Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa Endrew Scout alisema ameridhika na maelezo yaliyotolea na wakili wa serikali pamoja na vielelezo likiwamo gari lililotumiwa na watuhumiwa hao kusafirisha watu hao kutoka Kongowe Dar es Salaam ...

Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa Mhekwa Azindua Maadhimisho ya Miaka 39 ya CCM

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephram Mhekwa akihutubia wananchi wa Kijiji cha Lulanzi wilayani Kilolo, mkoani Iringa wakati sherehe za uzinduzi wa maadhimisho  kimkoa ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM. (Picha zote na Friday Simbaya) MAADHIMISHO ya kumbukumbu ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimkoa yamezinduliwa Januari 31, mwaka huu, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephraam Mhekwa katika Kijiji cha Lulanza wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa. Aidha, kilele cha maadhimisho hayo kinatarajiwa kufanyika mkoani Singida, Februari 6, mwaka huu, na mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais mstaafu Jakaya Kikwete. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephraam Mhekwa alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho kimkoa mgeni rasmi atakuwa mlezi wa mkoa ambaye ni waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Tanzania Mzengo Pinda. Alisema pia kuwa kilele cha maadhimisho hayo kimko...

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kundi la Mziki la Navy Kenzo Kutoa Wimbo na Video Mpya-Kamati

THE INDUSTRY MUSIC LABEL   TAARIFA KWA UMMA KUNDI LA MZIKI LA NAVY KENZO LATOA WIMBO/VIDEO MPYA-KAMATIA Baada ya kutamba Mwaka Jana Africa nzima na wimbo unaoitwa ‘Game’, Kundi la Navy Kenzo limeanza mwaka vizuri baada ya kutoa wimbo mpya pamoja na video yake unaitwa “Kamatia” , Wimbo huo umeshaanza kuwa gumzo sehemu mbali mbali na kuonyeshwa kwenye TV za kimataifa siku mbili tu baada ya kutoka, Uzinduzi wa Wimbo Huo ulifanyika Kiaina yake kwa Staili ya 'Flash Mob' Kwenye Club ya Rhapsody kwa kuwasuprise waliokuwa ndani ya Club hiyo. Kundi la Navy Kenzo linaloundwa na Aika na Nahreel mpaka sasa wameshatoa nyimbo kadhaa zilizotamba sana kama Moyoni, Bokodo, Visa na nyingine nyingi. Navy Kenzo wameamua kutoa Wimbo pamoja na Video yake moja kwa moja kutokana na ushindani uliopo kwa sasa kwenye Music wa Bongo Flava, Video imefanyika nchini South Africa na Muongozaji wa Video wa kimataifa anayeitwa Justin Campos. Kamatia ni wimbo ambao unaongelea kuhusu wapenzi wawili waliomua k...

Mfuko wa Dharura wa UN watoa Dola Milioni 11 kusaidia wakimbizi wa Burundi na jamii ya Tanzania

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ametoa dola za Marekani milioni 100 (US$ 100m, sawa na shilingi za Tanzania bilioni 220) kutoka katika Mfuko Mkuu wa Kushughulikia Dharura wa Umoja wa Mataifa (CERF) kwa shughuli za misaada katika maeneo tisa yenye dharura duniani na yasiyo na fedha za kutosha. Tanzania—ambayo kihistoria imepokea mamilioni ya wakimbizi kutoka nchi jirani kwa miaka mingi—imetengewa dola za Marekani milioni 11 (Sawa na shilingi za Tanzania bilioni 24) kutoka katika kiasi hicho kwa lengo la kushughulikia mahitaji ya wakimbizi kutoka Burundi. Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akitoa msaada katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo mkoani Kigoma wakati alipofanya ziara mkoani humo Zaidi ya raia 126,000 wa Burundi wamekimbilia nchini Tanzania tangu mwezi Aprili, 2015, kufuatia machafuko ya kisiasa nchini humo. Huku tayari wakimbizi 64,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) wakiwa tayari nchini. Tanzania hivi sasa ina zaidi ya wakimb...

Cameron's hopes of early EU referendum recede after talks with Tusk

PM and European council president fail to reach deal over renegotiation of Britain’s relationship with EU before crucial summit David Cameron and Donald Tusk meeting at No 10 to discuss the proposed ‘emergency brake’ on welfare payments for EU migrants. Photograph: Toby Melville/WPA Pool/Getty Images Rajeev Syal David Cameron’s preferred option of an early referendum on Britain’s membership of the EU edged further away after he failed to broker a deal with the president of the European council, Donald Tusk . The two men had hoped to finalise a renegotiation of Britain’s relationship with Brussels over dinner at Downing Street so that it could be put to other EU leaders on Monday ahead of a crucial summit in less than three weeks. An early deal would allow Cameron to call a referendum on the UK’s EU membership before the summer. But a Downing Street source said that none of the four key areas under negotiation have been agreed. Instead, further negotiations will be left to diplo...