SALAMU ZA MKUU WA MKOA WA IRINGA ZA KUWATAKIA HERI WANANCHI WA MKOA WA IRINGA KATIKA SHEREHE ZA NOELI NA MWAKA MPYA 2015
Ndugu Wananchi wa Mkoa wa Iringa Ninayo heshima kubwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetuwezesha tuwe na afya njema tokea tulipoanza mwaka 2014. Ni matumaini yangu kuwa Mungu atatuwezesha pia kuumaliza salama mwaka 2014 na hatimae kuuanza mwaka 2015.