Skip to main content

Posts

Showing posts from February 23, 2026

MBUNGE KIHENZILE AZINDUA KITUO CHA AFYA MAKUNGU CHA SH MILIONI 500

Mufindi. MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kusini, David Kihenzile , amezindua Kituo cha Afya cha Makungu kilichojengwa kwa gharama ya Sh milioni 500 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, hatua inayotarajiwa kumaliza changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya kwa zaidi ya wananchi 17,000 wa kata hiyo na maeneo ya jirani. Kukamilika kwa mradi huo kunatajwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 za mwanzo wa muhula wake mpya wa uongozi baada ya Uchaguzi Mkuu, ambapo Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya afya na kusogeza huduma karibu na wananchi. Akizungumza leo Februari 23, 2026, wakati wa ziara yake ya siku nne jimboni humo, Mbunge Kihenzile ambaye pia ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, alisema ujenzi wa kituo hicho ni mkombozi mkubwa kwa wakazi wa Makungu, Mgololo na maeneo ya jirani waliokuwa wakilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya, hususan huduma za mama na mtoto. Alisema kipindi cha mvua wananchi wa ukanda wa Mgolol...

Mawelewele Yafuta Daraja la Sifuri kwa Miaka Miwili Mfululizo

Iringa. Shule ya Sekondari Mawelewele iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imeandika historia mpya kwa kufuta daraja la sifuri kwa miaka miwili mfululizo katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne kwa shule za serikali. Hatua hiyo imetajwa kuwa mafanikio makubwa katika kuinua kiwango cha ufaulu na hadhi ya shule hiyo kitaaluma. Kutokana na matokeo hayo, shule imefanikiwa kushika nafasi ya pili ngazi ya halmashauri, ikiendelea kuonesha mwelekeo chanya wa kitaaluma na ushindani bora miongoni mwa shule za sekondari za manispaa hiyo. Mkuu wa shule hiyo, Mwl. Robert Ngimba, amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya walimu, wanafunzi na wazazi, pamoja na kuimarika kwa nidhamu, ufuatiliaji wa maendeleo ya wanafunzi na utoaji wa masomo ya ziada kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum. Ameeleza kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1998 na hadi sasa imekuwa na wakuu wa shule wanne waliomtangulia, yeye akiwa wa tano. “Shule yetu inaendelea kukua kitaalum...