Skip to main content

Posts

Showing posts from October 17, 2014

MWANRI: ZINGATIENI WELEDI WAKATI WA KUANDAA MAANDIKO YA MIRADI

  Kaimu Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (aliyesimama) akizungumza na baadhi ya viongozi waandamizi wizara za viwanda na biashara, fedha, uchukuzi, nishati na madini pamoja na viongozi waandamizi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Zanzibar.      Bibi Maryam Khamis (Wapili kulia) Mtaalam wa uchumi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Zanzibar akizungumza katika kikao hicho. Mmoja wa wajumbe wa kikao hicho, Bw. Aunyisa Meena kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara akichangia mada.

CHANJO YA SURUA-RUBELLA, MATENDE NA MABUSHA KUTOLEWA

Na Beatrice Lyimo- MAELEZO Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo inatarajia kufanya kampeni shirikishi ya ugonjwa wa Surua na Rubella kuanzia tarehe 18 hadi 24 oktoba, 2014.

Serikali ya Tanzania yapokea zaidi ya Sh. Bilioni 10

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Doroth Mwanyika (kushoto) akitia saini mkataba wa ushirikiano wa Mpango wa Mageuzi ya Usimamizi wa Fedha za Umma (PFM)  Awamu ya IV kwa niaba ya Serikali ya Tanzania leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Balozi wa Finland nchini Bi. Sanikka Antila.  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Doroth Mwanyika (kushoto) akibadilishana hati ya mkataba wa ushirikiano wa Mpango wa Mageuzi ya Usimamizi wa Fedha za Umma (PFM) Awamu ya IV waliosaini leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Balozi wa Finland nchini Bi. Sanikka Antila. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Bi. Doroth Mwanyika (kushoto) akishukuru Serikali ya Finland kwa ushirikiano mzuri wanaoendelea kuipa Tanzania mpaka sasa na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika katika malengo yaliyokusudiwa. Kulia ni Balozi wa Finland nchini Bi. Sanikka Antila. Balozi wa Finland nchini Bi. Sanikka Antila  (kulia)PFM akiongea na waandishi wa habari  (hawapo pichani) na kuipongeza ...

Renamo-hatutambui matokeo

Chama cha kikuu cha upinzani nchini Msumbiji cha RENAMO,kimetoa yake ya moyoni kuwa hawatayakubali matokeo yajayo ya uraisi na ubunge pamoja na serikali za mitaa. Msemaji wa chama hicho Antonio Muchanga amesema kwamba kumekuwa na ukiukwaji wa taratibu katika upigaji kura huo na udanganyifu wa kura. Matokeo ya awali katika uchaguzi huo zinaonesha kwamba chama cha FRELIMO kinaongoza katika uchaguzi huo.Wakati haya yakitokea kumekuwa na uvunjifu wa amani wakati polisi walipo ingia katika ghasia na waandamanaji waliokusanyika nje ya vituo vya kupigia kura kufuatilia zoezi la uhesabuji wa kura . Ingawa wafuatiliaji wa uchaguzi nchini Zimbabwe wanaeleza kuwa pamoja na yote hayo,uchaguzi huo ulikua huru na wa haki.ikumbukwe kuwa chama cha Renamo na chas Frelimo walipigana vita ya wenyewe kwa wenyewe vilivyomalizika mnamo mwaka 1982.(BBC)