Skip to main content

Posts

Showing posts from September 28, 2015

MAGUFULI AZIDI KUCHANJA MBUGA KAMPENI ZAKE ZAINGIA MKOA WA IRINGA

Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wakazi wa Mafinga kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika viwanja vya Wambi Mafinga ambapo aliwaambia wakazi hao wasihadaike na maneno ya kisiasa yanayotolewa na vyama vingine kuwa nchii hii haijapiga hatua wakati maendeleo yanaonekana wazi na nchi inazidi kusonga mbele. Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa Mafinga kwenye mkutano wa kampeni za CCM. Mgombea ubunge wa Jimbo la Mafinga Cosato Chumi akihutubia wakazi wa mji huo wakati wa mkutano wa kampeni ambapo Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli alihutubia pia. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mafinga Cosato Chumi akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa kampeni za CCM ambao ulihutubiwa pia na mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM...

Endometriosis: the hidden suffering of millions of women revealed

  Primary care doctors often do not know what endometriosis is and large numbers of women are under-treated or badly treated for the disease. Photograph: Alamy Stock Photo Sarah Boseley , Jessica Glenza and Helen Davidson The hidden toll and extraordinary neglect of a disease that affects an estimated 176 million women around the globe, causing many to suffer a life of pain and debilitation and sometimes infertility, is revealed by the Guardian. One woman in 10 of reproductive age has endometriosis, it is estimated, and yet often their primary care doctors do not know what it is and the specialists to whom they are sent are ill-informed. Vast numbers of women are under-treated or badly treated. It can take years to get a diagnosis and during that time women may suffer severe pain and are unable to work, socialise or maintain a sexual relationship. What is endometriosis? A visual guide Read more The disease does not always have symptoms a...

DStv YAJA NA CHANELI YA MAISHA MAGIC BONGO, KWA AJILI YA WATANZANIA

Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa kubwa la kuonesha vitu mbalimbali vinavyoburudisha katika chaneli za DStv na GoTv kupitia MultiChoice hivi karibuni nchini Mauritius. Mkurugenzi wa M-Net kwa nchi za Afrika Mashariki na SADC, Theo Erasmus akifurahi jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi mbalimbali za Afrika. Na Modewjiblog , Mauritius Moja ya makampuni yanayoongoza katika utoaji wa vipindi vya burudani barani Afrika M-Net imesema kwamba itazindua chaneli maalumu kwa ajiri ya wakazi wa Tanzania itakayojulikana kama maisha Magic Bongo. MAISHA MAGIC BONGO itaruka hewani kupitia chaneli 160 ya DStv kuanzia Alhamisi ya Oktoba Mosi mwaka huu na itapatikana katika vifurushi vyote vya Access, Family, Compact, Compact Plus na Premium. Imeelezwa kuwa ingawa mambo yametengenezwa mahsusi kwa ajili ...

INAWEZEKANA KUPIGA VITA UMASKINI KWA USHIRIKIANO-UN

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini (SDG’s) Tanzania katika shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla ambayo pia benki ya Standard Chartered Tanzania ilishiriki na kugawa vitu mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. (Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog ) Na Mwandishi wetu Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, amesema uondoaji umaskini nchini unawezekana kwa ushirikiano kati ya wadau mbalimbali wa maendeleo. Kauli hiyo ameitoa mwishoni mwa wiki wakati akizindua Malengo Endelevu 17 ya Maendeleo nchini (SDG’s) Tanzania katika shule ya Uhuru mchanganyiko, katika hafla ambayo pia benki ya Standard Chartered ilishiriki na kugawa vitu mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo. Katika hafla hiyo ambayo ilitengenezwa mahususi kua...