Skip to main content

Posts

Showing posts from October 27, 2011

ASKOFU SIMALENGA AZUILIWA KUINGIA KANISANI KWA TUHUMA ZA WIZI WA VIFAA VYA BILIONI MOJA (1BN/=), MTIKILA ASEMA YUKO TAYARI KUONESHA VILIPO.

Na Mwandishi Wetu, Ludewa TUHUMA za ubadhilifu wa vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja zinazomkabili Askofu John Simalenga wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Southwest Tanganyika Njombe, umechukua sura mpya baada ya waumini wenye hasira kumzuia kuendesha Ibada Milo. Dhahama hiyo ilimpata mchungaji huyo wa kiroho Oktoba 23, 2011katika Kanisa la Kung’aa kwa Bwana lililoko Mtaa wa Milo wilayani Ludewa mkoani Iringa, alikokwenda kuendesha Ibada ya Kipaimara. Awali waumini hao walimsimamisha kazi mchungaji wa mtaa wa Milo Padre Jophrey Mturo na kumnyima mshahara kwa madai kuwa ameshiriki ubadhirifu huo ndiyo maana amekuwa akimtetea Askofu huyo. Hata hivyo, Padre Mturo alilazimika kufungasha mizigo yake siku hiyohiyo na kukimbilia Kijiji cha Mlangali kwa hofu ya kuvamiwa na waumini wenye hasira na kwamba anasubiri maelekezo ya Askofu kuhusu kupangiwa kituo kingine cha kazi. Wakizungumza kanisani hapo waumini na viongozi wa mtaa huo walisema wameamua kumzuia mlango...