Na Friday Simbaya,
S ongea
PAROKO Padre Joseph Ndimbo wa Parokia ya Peramiho Jimbo Kuu
la Songea aliwaasa waombolezaji kuacha
mara moja tabia kugombeana maeneo ya kuzika marehemu.
Alisema kuwa kuna mtindo umezuka wanandugu kuvutana wapi
wamzike marehemu na kuongeza kuwa huku ni kumdhalilisha marehemu.
Pd. Ndimbo alisema hayo Jumamosi wakati wa mazishi ya aliyekuwa
mwenyekiti wa Tanzania labour Party (TLP)wilaya ya Songea, Bw. Kalo Kombe
katika makaburi ya Liangano karibu na Kijiji cha Lipinyapinya Kata ya Peramiho.
Alisema kuwa sio tabia nzuri kwa wanandugu kugombeana maiti
, kumbe maeneo yote yanafaa kuzikia.
“Imezuka tabia katika jamii ya watu kugombania maiti yaani
mvutanao wa watu wawili kugombania maiti wakati wa mazishi kila mtu anataka kuzika mahali pake, huku
kote ni kuhangaika na kumtesa marehemu. Kuzikwa ni kuzikwa tu hata kama
atazikwa Peramiho ‘A’ au Peramiho ‘B’,” alitoa mfano...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.