Skip to main content

Posts

Showing posts from June 26, 2011

MWENYEKITI TLP SONGEA AFARIKI DUNIA

Na Friday Simbaya, S ongea PAROKO Padre Joseph Ndimbo wa Parokia ya Peramiho Jimbo Kuu la Songea aliwaasa  waombolezaji kuacha mara moja tabia kugombeana maeneo ya kuzika marehemu. Alisema kuwa kuna mtindo umezuka wanandugu kuvutana wapi wamzike marehemu na kuongeza kuwa huku ni kumdhalilisha marehemu. Pd. Ndimbo alisema hayo Jumamosi wakati wa mazishi ya aliyekuwa mwenyekiti wa Tanzania labour Party (TLP)wilaya ya Songea, Bw. Kalo Kombe katika makaburi ya Liangano karibu na Kijiji cha Lipinyapinya Kata ya Peramiho. Alisema kuwa sio tabia nzuri kwa wanandugu kugombeana maiti , kumbe maeneo yote yanafaa kuzikia. “Imezuka tabia katika jamii ya watu kugombania maiti yaani mvutanao wa watu wawili kugombania maiti wakati wa  mazishi kila mtu anataka kuzika mahali pake, huku kote ni kuhangaika na kumtesa marehemu. Kuzikwa ni kuzikwa tu hata kama atazikwa Peramiho ‘A’ au Peramiho ‘B’,” alitoa mfano...