Skip to main content

Posts

Showing posts from October 6, 2017

BOT YAPIGA MSASA VIZIWI MKOANI IRINGA KUHUSU NOTI HALALI

IRINGA: Viziwi mkoani Iringa wameishukuru Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kuendesha mafunzo ya elimu ya umma ya utambuzi wa alama za usalama za noti halali.  Walemavu hao walitoa kauli hiyo jana kwenye risala iliyosemwa mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza, ambapo jumla ya viziwi 50 walipatiwa mafunzo ya utambuzi wa alama za usalama za noti halali.  Walisema kuwa semina hiyo ni muhimu sana kwao kwa sababu itawawezesha kutambua noti halali na halisi kwa walemavu wa kusikia mkoani Iringa.  Mafunzo hayo yaliandaliwa na kituo cha sanaa na utamaduni kwa viziwi Tanzania (KISUVITA) kwa kushirikiana na Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) mkoa wa Iringa.  Akisoma risala mwenyekiti wa KUSUVITA, Habibu Mrope kwa niaba ya walemavu alishukuru BOT kwa kuwezesha mafunzo ikiwa ni mwendelezo wa zile, ambazo zimekwishafanyika katika mikoa ya Lindi, Dodoma, Singida, Ruvuma, Njombe, Shinyanga, Simiyu, Mwanza, Mara, Kigoma, Tabora na Kagera tangu mwaka...

AMKA NA MAGAZETI NA TUMBUSI BLOG (ZAMANI SIMBAYABLOG)

Ni asubuhi nyingine tena nakukutanisha na habari kubwa kwenye Magazeti ya Tanzania leo October 7 2017 kuanzia ya Udaku, Michezo na Hardnews.

DKT HELEN KIJO BISIMBA AMTEMBELA TUNDU LISSU

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dkt Helen Kijo Bisimba (Pichani) amesafiri mpaka Nairobi nchini Kenya kwenda kumjulia hali Mbunge Singida Mashariki, Tundu Lissu. ambapo anapatiwa matibabu baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana Mjini Dodoma. Mwanaharakati huyu maarufu nchini ,katika safari yake hiyo , aliongozana na watetezi wenzake na haki za Binadamu ambapo mara baada ya kumjulia hali Lissu ambaye ni Rais wa chama cha wanasheria nchini,(TLS) , amesema haya "Leo Mungu amenipa neema kumuona Mh. Tundu Antipas Mughway Lissu nimeuona kwa macho muujiza kuwa Tundu pamoja na marisasi yale yote ameniona na kuniamkia nakunipa pole. Yaani yeye ndio anatupa sisi moyo kuwa Kufa mtu hufa mara moja tusiogope kusimamia haki, " Pichani ni Mkurugenzi wa (LHRC)Dk Bisimba akiwa na watetezi wenzange mjini Nairobi Kenya Ameongeza kusema kuwa "kusema ukweli, kutetea wanaoonewa.Nimepata nguvu mpya.Watanzania Tundu anawa...