Skip to main content

Posts

Showing posts from January 11, 2017

Mwenyekiti mpya wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Arusha (ARFA) Peter Temu

Na Woinde Shizza,Arusha Chama cha soka Mkoa wa Arusha (ARFA) kimefanikiwa kupata uongozi mpya baada ya uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika mwishoni mwa wiki Wilayani Monduli ambao watakaa madarakani kwa miaka minne. Katika uchaguzi huo uliokuwa unawaniwa nafasi kumi, ulionekana mgumu kwa nafasi mbili pekee ile ya Mwenyekiti pamoja na nafasi ya Mjumbe wa mkutano mkuu wa TFFambapo wagombea walikua wawili wawili. Waliofanikiwa kupita katika uchaguzi huo kwa nafasi ya mwenyekiti ni Peter Temu aliyemshinda Omary Walii kwa kura 13 kwa 6, Katibu mkuu Zakayo Mjema aliyepata kura 18, katibu msaidizi akipitaNassoro Mwarizo. Nafasi ya Mweka hazina ikienda kwa Omary Nyambuka, Huku nafasi ya Mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF Issa Hamisi alimshinda Athumani Mhando kwa kura 13 kwa 8, na nafasi ya kamati tendaji ya ARFA ikienda kwa Soud Abdy. Washiriki ambao ni wajumbe wa vyama vya soka kutoka Mkoani hapa waliojitokeza ni kutoka Arusha Mjini, Monduli, Arume...

JPM ASEMA TANZANIA HAINA NJAA, NI PROPAGANDA ZA WANASIASA NA...

HOTUBA YA RAIS MAGUFULI LEO SIMIYU.  Rais Dk. John Magufuli leo hii akiwa mkoani Simiyu amesema kwamba Tanzania hakuna njaa na kwamba anayejua kama nchi ina njaa ni yeye mwenyewe. "Anayejua kuna njaa nchi hii ni Rais, mimi ndiyo ninayejua wapi kuna njaa na wapi hakuna.Tanzania hii haina njaa wala watu hawana njaa," anasema Rais JPM kutoka Simiyu "Wanaotangaza kuna njaa ni watu wanaolipwa pesa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema nchi ina njaa na ukame wa kuua watu na mifugo. "Yapo magazeti yanayotumiwa na wafanyabiashara na wanasiasa ili kusema Tanzania kuna njaa. Kuna mfanyabiashara mmoja ana tani elfu 25 za mahindi bandarini anataka aingize bila kodi kwa kisingizio cha njaa Tanzania," amesema. Rais anasema ameagiza alipe kodi na asipitishe mahindi hayo bure kwa kisingizio cha njaa, kwa sababu Tanzania haina njaa. "Kuna mfugaji mwingine walimlipa hela wanasiasa huko Mvomelo,akaenda mbele ya TV na kusema ana mifugo inaku...