Mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd, Salim Asas Abri (aliyesimama) akitoa maelezo ya kiwanda cha kuzalisha maziwa na bidhaa zake kilichopo mkoani Iringa kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Titus Kamani wakati ya ziara ya kutembelea nyanda za juu kusini kupitia mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa afrika ya mashariki awamu ya pili. Mradi wa uendelezaji sekta ya maziwa afrika mashariki (East Africa Dairy Development) ni mradi wa miaka mitano (2013-2018) unatekelezwa kwa awamu ya pili katika nchi za Kenya, Uganda na tanzania kwa mfumo wa kitovu cha maziwa (dairy hub). Nchini tanzania mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambao unatekelezwa kwa ubia-kongano (consortium partnership) kati yaa Heifer International (msimamizi mkuu wa mradi na kuongoza uzalishaji maziwa) kwa kushirikiana na Technoserve (biashara na masoko ya maziwa). Mitamba katika shamba la Kibebe linalomilikiwa na Richard Phillips lillilopo ka...