Skip to main content

Posts

Showing posts from January 22, 2014

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA INA JUMLA YA WANAFUNZI 3770 WASIOJUA KUSOMA, KUANDIKA NA KUHESABU

  Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Mkilikti akifungua mkutano wa siku moja wa wadau wa elimu wa tathmini ya elimu na matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na daras la nne mwaka 2013 leo katika Ukumbi wa Mt. Benedkito Peramiho wilayani Songea, mkoani Ruvuma.   Wadao elimu mbalimbali wakimsikiliza mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Mkilikiti wakati mkutano wa tathmini wa kuhitimu elimu ya msingi na darasa la nne mwaka 2013wilayani Songea, mkoani Ruvuma leo. Na Friday Simbaya, Songea Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma katika Idara ya Elimu ya Msingi   ina jumla ya wanafunzi 3770 wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu (K.K.K.), imefahamika. Hayo yalibainika wakati   wa mkutano wa kutathmini elimu na matokeo ya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi na daras la nne mwaka 2013 uliofanyika hapa Peramiho hivi karibuni . Akisoma taarifa yake ya utekelezaji kwa wadau wa elimu mbalimbali waliohudhuria kikao hic...

WATANZANIA MILIONI 5 HATARINI KUTOPIGA KURA MWAKANI

Na Friday Simbaya, Songea Katibu Mkuu wa Chadema Dkt. Wilibrodi Slaa amesema zaidi ya watu milioni tano (5m) nchini Tanzania hawataweza kushirika kupigakura ya maoni ya katiba ya rasimu ya pili kwa  kupigiakura kutokana na mbalimbal ikiwemo kukosa shahada za kupigiakura imefahamika. Dkt. Slaa alisema kuwa watu wengi waliofikisha miaka kumi na nane (18) na waliopoteza shahada hizo ama kwa kuuza au kupoteza hawatashirika kupigakura ya maoni ya katiba. Hayo yalisema leo wakati wa Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Tamasha vilivyopo Namihoro, wilayani Songea vijijini mkoani Ruvuma, wakitokea Mbamba Bay na Mbinga, ikiwa ni kuashilia mwanzo wa opresheni M4C PAMOJA Daima inayofanyika nchini nzima. Alisema ili watu wengi waweze kushiriki kupigakura ya maoni ya katiba kikamilifu ni lazima daftari ya wapigakura nchini liboreshwe. “Tunaiomba serikali kupitia Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC) ianze zoezo la kuboresha daftari ya wapigakura ili watu wengi washiriki...