Skip to main content

Posts

Showing posts from October 22, 2014

Mizengo Pinda kuwania Urais

Waziri Mkuu , Mizengo Pinda, ametangaza nia yake ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao . Pinda aliyasema hayo mjini London ambako mkutano wa viongozi unaoangazia uwekezaji zaidi katika bara la Afrika unaendelea . Viongozi hao wanatumaini kuyashawishi mashirika makubwa zaidi ya uwekezaji, katika mkutano huo wa siku mbili, kwamba yanafaa kuwekeza zaidi katika mataifa ya Afrika, hasa Nigeria, Uganda, Tanzania, Rwanda, Ghana na Togo. (BBC)

Chuo Kikuu Ardhi kutatua tatizo la udhibiti wa maji taka na taka ngumu

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi Prof. Idrissa Mshoro akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mpango wa chuo hicho wa kuendelea na jitihada za kutatua tatizo la udhibiti wa maji taka na tanga ngumu ikiwemo ujengaji wa miundombinu ya majaribio ya teknolojia za kibiolojia zinazobadili tanga ngumu au maji taka ambayo huzalishwa majumbani kuwa mboji na gesi asili ya kupikia, wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma wa chuo hicho Prof. Gabriel Kassenga Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Ardhi ambaye pia ndiye mtaalam wa teknolojia za kibiolojia zinazobadili tanga ngumu au maji taka (waste treatment facilities) Dkt. Shabaan Mgana Akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani) namna Teknolojia hiyo ya kubadili taka ngumu na maji taka inavyotumika na kuwasaidia wananchi walioonesha nia ya kuitumia ikiwamo kupata mboji kwa ajili ya mazao, mimea pamoja na kupata gesi asili ya kupikia, ambapo mpaka sasa k...

MAGAZETI JUMATANO