Wananchi wa Mtaa wa Mwambisi wakifua kwa kutumia maji ya mabondeni Wakazi wa Mtaa wa Mwambisi Kata ya Kongowe iliyopo wilayani wakichota maji ya mabondeni kutokana na maji safi na salama katika kata hiyo kutoka mara moja kwa wiki na kusababisha kero na hofu kwa watumiaji wa maji hayo. Picha zote na Elisa Shunda Mmiliki wa Blog ya Shunda Blog,Elisa Shunda, akichota maji kwa ajili ya matumizi ya kuoga Wananchi wa mtaa huo wakielekea katika eneo la Bonde la Miti Mirefu kuchota maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kama kufulia nguo,kupikia na kunywa jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa afya yao. NA ELISA SHUNDA,KIBAHA Serikali imeombwa kuingilia kati suala la ukosefu wa upatikanaji wa maji safi katika kata ya Kongowe eneo la Mwambisi ambalo maji yamekuwa yakitoka mara moja kwa wiki na kusababisha wananchi kutumia maji ya mabondeni yasiyo salama kwa matumizi ya binadamu. Wakizungumza na Raia Tanzania,jana wakazi wa maeneo mbalimbali w...