Skip to main content

Posts

Showing posts from January 4, 2017

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI

KIGOMA SISTERS FC YAIBAMIZA PANAMA FC YA IRINGA 2-1

Kigoma Sister FC ya Kigoma (jezi la bluu) yaichapa Panama FC ya Iringa bao 2-1 katika mechi iliochezwa katika Uwanja wa Kumbukumbu wa Samora mjini Iringa leo, katika Ligi ya Wanawake inayoendelea nchini . Katika kipindi cha kwanza timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufanya goli 1-1, lakini katika kipindi cha pili upepo ulibadilika kwa timu ya Kigoma Sister kuongeza goli la pili. Timu zingine zinazoshiriki ligi hiyo ni Viva Queens ya Mtwara, Fair Play FC (Tanga), Mlandizi Queens (Pwani), Marshi Academy (Mwanza) na Baobao Queens (Singida).  Zingine ni JKT Queens (Bukoba), Mburahati Queens na Evergreen Queens zote za jijini Dar es Salaam. Chama cha soka la wanawake Tanzania (TWFA)kwa kushirikiana na Shirikisho la soka Tanzania (TFF) kinaendesha ligi hiyo.

LIPULI FC, ‘YATEMBEZA BAKULI’

Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango na Fedha wa Timu ya Lipuli FC, Jullie Sawani (kulia) akizungumza na waandishi wa habari mjini Iringa leo (jana) kuhusu mikakati yao ya kupandisha timu Ligi Kuu. Lipuli Football Club, imeanza safari yake vizuri yenye matumaini kuelekea Ligi Kuu Bara, kwa hiyo kamati imewaomba wadau mbalimbali nje na ndani mkoa wa Iringa kuichangia timu hiyo kupande daraja.  Baadhi wa wachezaji wa Klabu kongwe ya Lipuli Football Club yenye makazi yake katika Mji wa Iringa wakiwa katika kambi yao iliyopo katika Hoteli ya Sambala mjini Iringa jana. Kushoto ni nahodha wa timu hiyo Ally Sonso, timu hiyo ipo kambini kwa ajili ya mechi yao dhidi ya timu ya Mshikamano ya jijini Dar es Salaam Jumamosi wiki hii.  Duru la Kwanza Lipuli FC vs African Sports 1-1 Lipuli FC vs Kiluvya 1-0 Lipuli FC vs Pamba 2-0 Mshikamano vs Lipuli 0-1 Polisi vs Lipuli 0-1 Friends Rangers vs Lipuli 3-0 Ashanti vs Lipuli 1-1 Duru la Pili African ...