SIMBA NA YANGA ZAKUTANA MARA 81, NANI ATASHEREHEKEA! Na Daniel Mbega JUMAMOSI hii Februari 20, 2016 bingwa wa ‘kucheka na nyavu’ wa miaka yote Uingereza, James Peter ‘Jimmy’ Greaves, atakuwa anasherehekea miaka 76 ya kuzaliwa kwake, lakini kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kutakuwa na habari nyingine wakati mahasimu wakuu wa soka Tanzania, Yanga na Simba watakapokuwa wakivaana kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Timu hizo zinapambana katika siku ya 51 ya mwaka, lakini ni baada ya siku ya 112 tangu zilipopambana mara ya mwisho – katika mchezo wa kwanza wa msimu wa 2015/2016 – Septemba 26, 2015 kwenye uwanja huo huo na Yanga wakaibuka washindi kwa mabao 2-0 wakilipa kisasi cha kufungwa ‘bao la kizembe’ na pekee Machi 8, mwaka huo lililopachikwa kimiani na Emmanuel Okwi. Achana na akina Alan Shearer, Wayne Rooney na Thierry Henry, mkongwe Greaves ndiye mchezaji pekee aliyefunga mabao mengi zaidi kwenye ligi ya juu (top flight) wakati huo ikiw...