Skip to main content

Posts

Showing posts from August 31, 2014

LHRC WAGAWA CD, FLASH DISK,VIPEPERUSHI PAMOJA NA RANDAMA BURE...!

Mkazi wa Kihesa katika Manispaa ya Iringa, Peter Kalawa akiuliza swali katika mkutano wa hadhara wa Kampeni ya Kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC) ya kusambaza uelewa juu ya Katiba kwa wananchi uliyofanyika Kihesa Sokoni hivi karibuni. Wakati wa mkutano CD za sauti ambako Rasimu ya Pili ya Katiba imerekodiwa yote kwa lugha nyepesi, "flash disk" kwa ajili ya madereva wa Bodaboda na machapisho kwa lugha nyepesi vilitolewa bure .(PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) Wakazi wa Kihesa katika Manispaa ya Iringa, wakifuatilia kwa umakini mkutano wa hadhara wa Kampeni ya Kituo cha Sheria na haki za Binadamu (LHRC) ya kusambaza uelewa juu ya Katiba kwa wananchi unaendelea katika mikoa 20 ya Tanzania bara na visiwani, uliyofanyika Kihesa Sokoni hivi karibuni. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)

CCM YAIBOMOA NGOME YA CHADEMA

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga akipokea kadi ya CHADEMA kutoka kwa Desius Nyoni (kushoto) aliyekuwa Afisa Habari Msaidizi Wilaya ya Mufindi katika mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika katika Kijiji cha Nyololo, mkoani Iringa jana.