Skip to main content

Posts

Showing posts from November 20, 2017

CCM YAONGEZA NGUVU KAMPENI ZA UDIWANI KITWIRU

HUKU kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kitwiru zikiingia wiki ya lala salama, Chama cha Mapinduzi (CCM) kinazidi kuongeza nguvu katika kampeni zake kwa kuwapandisha jukwaani makada mbalimbali wanaonadi sera za chama hicho na kumuombea kura mgombea wao, Baraka Kimata. Baraka Kimata anayepewa nafasi ya kushinda uchaguzi huo kama ilivyo kwa mshindani wake kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Bahati Chengula amesema ameamua kuigeuka Chadema na kujiunga na CCM ili apate fursa pana zaidi ya kuwatumikia wananchi wa kata hiyo. Kimata alikuwa diwani wa kata hiyo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kupitia Chadema kabla ya kujiengua akipinga kile anachodai udikteta wa Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa. Katika uchaguzi mkuu wa 2015, Kimata alishinda udiwani wa kata hiyo kupitia Chadema akipata kura 3,183 dhidi ya kura 2,557 alizopata mgombea wa CCM.

MCHUNGAJI MSIGWA ANOGESHA KAMPENI ZA UDIWANI KITWIRU

MBUNGE wa Jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msingwa (CHADEMA) amesema chama chao kimemsimamisha mgombea makini, mwenye uwezo na mchapakazi hodari anayeweza kushirikiana vyema na wananchi wa kata ya Kitwiru kuleta maendeleo. Katika uchaguzi huo mdogo utakaofanyika Novemba 26, mwaka huu Chadema imemsimamisha Bahati Chengula dhidi ya mgombea wa CCM, Baraka Kimata anayetuhumiwa kwa usaliti baada ya kukihama chama hicho. Msigwa anasema Baraka Kimata hakuwa mwanasiasa na ndio maana alihama kutoka Chadema akiwa na wadhifa wa udiwani na kukimbilia CCM ambako pia anatafuta nafasi ile ile. “Huyu mtu tulimuokota Ipogolo akiwa anashona nguo na alikuwa hajui chochote kuhusu siasa, tulimpika, akaanza kumudu jukwaa, akashinda udiwani, lakini kwa uroho wake wa fedha akahama Chadema. Anataka kuwatumia watu wa Kitwiru kujaza tumbo lake,” alisema Msigwa. Msigwa aliwaomba wana Kitwiru kumchagua Bahati Chengula akisema atakuwa katika nafasi nzuri ya kushirikiana na ...

KK to Zimbabwe to persuade Mugabe to step down

FILE: Hifikepunye Pohamba (l), Robert Mugabe (c) and Dr Kenneth Kaunda at Edgar Lungu’s inauguration Reuters reports that former president Kenneth Kaunda to Harare to try to convince President Robert Mugabe to step down in a “dignified exit” after the military seized power last week. The ruling party removed Mugabe as Zanu-PF president and first secretary on Sunday and lawmakers from the ruling party were due to meet at the party headquarters on Monday to discuss impeaching the 93-year-old leader. “Dr Kaunda used the presidential jet and has already arrived in Harare,” a senior government source told Reuters. Kaunda is also 93 years old. Botswana President Ian Khama has also called on Zimbabwe President Robert Mugabe to end his attempts to remain in office. The military intervention, which political sources say could pave the way to a national unity government after 37 years of Mugabe rule, also presented “an opportunity to put Zimbabwe on a path to peace ...