Skip to main content

Posts

Showing posts from May 13, 2011

CHADEMA WATIKISA MKOA WA RUVUMA KWA KUFANYA MAANDAMANO MAKUBWA!

Maandamano ya pikipiki yakitembea kutoka maeneo ya Msamara (Hoteli ya Top One Inn) kuelekea viwanja vya shule za msingi vya Kiburang'oma na Mloweka kupitia Barabara ya Peramiho. Maandamano hayo yalitembea zaidi ya kilometa 10 kuelekea Kata ya Lizaboni Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma yaliyoanza saa 9 alasiri leo . Maandamano yakipita katikati ya mjini wa Songea karibu na Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo mikoani. Kina mama nao hawakuwa nyuma kwa kutembea kilometa 10 kutoka Hoteli ya Top One Inn hapo Msamara walipofikia viongozi mbalimbali wa Chadema kuelekea Lizaboni kupitia barabara ya Peramiho na maadamano hayo yaliishia viwanja vya shule ya msingi ya Kiburang'oma kwa ajili mkutano wa hadhara. Viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiongoza maandamano wakiwemo M/kiti Freeman Mbowe, Katibu Mkuu Dr. Wilbroad Slaa, Naibu Katibu Zitto Kabwa na wabunge mbalimbali wa chama hicho. Wakazi wa Manispaa ya Songea na maeneo ya jirani wakifuatilia mkutano wa C...