Skip to main content

Posts

Showing posts from May 6, 2011

SIKU YA MALARIA DUNIANI IMANI ZA KISHIRIKINA ZA CHANGIA KUONGEZEKA KWA VIFO

Na Friday Simbaya, Ludewa WAKATI Taifa likishehekea mafanikio ya kuudhibiti ugonjwa hatari wa Maralia kwa kugawa vyandarua kwa mama wajawazito na watoto walio na umri chini ya miaka mitano Mkoani Iringa bado vyandarua havitoshi, lakini vilivyopo vinatumika kujifunika kama blanketi kujikinga na baridi imefahamika. Hayo yalithibitika hivi karibuni katika kijiji cha Mbwila Kata ya Luana Ludewa Mkoani Iringa wakati wa maadhimisho ya siku ya malaria kimkoa ambapo mkuu wa wilaya ya Ludewa Bi Georgina Bundalla alimwakilisha Mkuu wa Mkoa huo kama mgeni rasmi. Desmola Salo (37) aliliambia gazeti hili kuwa vyandarua vinavyotolewa na serikali havitoshi. “” mimi mwenyewe pale nyumbani ninayo familia ya watoto watano, lakini tunacho chandarua kimoja tu ambacho tunakitumia mimi na mume wangu huku watoto wakilala bila chandarua.”” Alilalamika Bi Desmola Kwa upande wake Bi Evelina Haule (65) na Pendo Kayombo wao walikiri kupokea vyandarua vyenye dawa kutoka kwa mawakala wa mabadiliko katika jam...

ASASI NYINGI NCHINI ZIMO HATARINI KUFA

MASHIRIKA yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) yamo hatarini kufunga milango ya ofisi zao kutokana na viongozi wengi wa mashirika hayo kukosa kabisa utaalamu wa kuandika miradi mbalimbali kwa ajili ya huduma za kijamii na badala yake yanasubiri wafadhili wenyewe wajitokeze jambo ambalo ni gumu sana kwa wafadhili kufanya hivyo imefahamika. Hayo yalijitokeza jana katika semina ya siku tano ya kuwajengea uwezo viongozi wa mashirika hayo yasiyo ya kiserikali wilayani Ludewa iliyofanyika katika ukumbi wa MTC Mlangali na kuandaliwa na Ludewa Non Governmental Umbrella (LUNGOU) chini ya ufadhili wa The Foundation for civil society ya jijini Dar es salaam. Pamoja na kuyajengea uwezo mashirika hayo juu ya uandaaji na uandishi wa miradi ya kijamii LUNGOU pia ili iliendesha semina ya ufahamu juu ya utawala bora ndani ya mashirika hayo na katika watumishi na wafanyakazi na watendaji ndani ya serikali na vyombo vya umma. Akifungua semina hiyo Afisa maendeleo ya jamii wilayani Ludewa Bw. William M...

MEI MOSI WAFANYAKAZI LUDEWA WAKERWA NA KIBURI NA KEJELI...

.Waajiri na Wakuu wa idara wakwepa kujitokeza kwenye sherehe hizo. MAADHIMISHO ya sherehe za mei mosi yanayofanyika kila mwaka duniani kote yamewachefua wafanyakazi nchini hususani Wilayani Ludewa kutokana na viongozi na baadhi ya wakuu wa idara kupuuza na kuchelewesha maslahi na stahili za wafanyakazi wa kada za chini. Akisoma risala kwa niaba ya wafanyakazi wote mwenyekiti wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Wilayani Ludewa Mkoani Njombe Bw Joseph Thomas Mvanga alisema waajili wanakatisha tamaa wafanyakazi wao na kusababisha kufanyakazi chini ya kiwango. Bw Mvanga alizitaja kero hizo kuwa ni pamoja na kuchelewesha mishahara yao ya kila mwezi, kutopandishwa vyeo kwa wakati, mazingira mabaya ya kufanyia kazi, viongozi na waajili kutoa lugha chafu na kejeli kwa wafanyakazi wa kada ya chini, wastaafu kucheleweshewa mafao yao kunapelekea wastaafu waatarajiwa kukata tama na kuingiwa na hofu kila wanapokaribia kustaafu hasa wanapoona mateso wanayopata waliotangulia. Naye...

WASOMALI 87 KIZIMBANI KWA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI

WAKIMBIZI 87 wa kabila la wahadia kutoka nchini Ethiopia wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wilayani Ludewa kwa kosa la kuingia nchini kwa makusudi bila ya kibali chochote huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria. Waethiopia hao ambao idadi yao kubwa ni wakristo na muislamu mmoja walikamatwa huko mwambao wa ziwa Nyasa katika kijiji cha Ngelenge Manda wakiwa wanajaribu kuvuka ziwa kwenda nchi jirani ya Malawi ambako wanakwenda kuomba hifadhi kutokana na kukimbia machafuko ya kisiasa nchini kwao. Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu mkazi wa mahakama ya Wilaya ya Ludewa Emanuel Mwambeta (DM) mwendesha mashtaka mratibu msaidizi wa polisi ambaye ni Mkuu wa upelelezi wilaya ya Ludewa ASP Thomas Mtikatika aliiambia mahakama hiyo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo April 13 mwaka majira ya tano asubuhi huko Ngelenge Manda mwambao wa ziwa Nyasa. Bw Mtikatika aliendelea kuiambia mahakama hiyo kuwa wakimbizi hao wamevunja sheria chini ya kifungu na 31 (1) (i) sheria namba 7 y...