WATANZANIA WALIVYOTUMIA FURSA YA TUKIO LA KUPATWA KWA JUA KUFANYA BIASHARA NA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII
Wafanyabiashara wa tikiti maji wakitumia tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali kuuza matunda hayo kwa wananchi waliofika katika eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa Jua. Wafanyabiashara wa Mchele wao pia hawakubaki nyuma wakatumia fursa hiyo kuuza Mchele kwa wananchi waliofika kushuhdia tukio hilo. Mama lishe pia hawaubaki nyuma kuhakikisha wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo . Benki ya NMB pia walitoa huduma ya kufungua Akaunti kwa wananchi waliofika katika eneo hilo kwa ajili ya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua. Umati mkubwa wa wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yaiendelea katika eneo hilo. Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ,Amosi Makala akizungumza juu ya fursa za kiuchumi zilizojitokeza kutokana na tukio la kupatwa kwa jua katika mji wa Rujewa wilayani Mbarali. Mkuu wa Mkoa wa Songe Luteni Mstaafu ,Chiku Galawa akizungu...