SHULE ya Kimataifa ya Iringa imetoa wito kwa serikali ya Dk John Magufuli kuanzisha mpango maalumu wa uingizaji na utumiaji wa teknolojia mbalimbali mpya kwa maendeleo ya nchi kwa kutoa ufadhili wa elimu kwa makundi mbalimbali ya wanafunzi watakaoplekwa katika nchi zenye teknolojia hizo. Pamoja na mpango huo, shule hiyo imeiomba serikali hiyo kutumia utajiri wa gesi ya Mtwara kuendelea kuboresha mazingira na mifumo ya utoaji wa elimu nchini ili iwiane na nchi zilizopiga hatua kubwa katika sekta hiyo. Hayo yalisemwa na mjumbe wa bodi ya shule hiyo, Edwin Port kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya shule hiyo yenye wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari zaidi ya 100, yaliyofanyika shuleni hapo juzi. Mkuu wa Utawala wa shule hiyo, Jean Milliken alisema; “Kwasababu shule yetu ni ya kimataifa, tumekuwa na kawaida kila mwaka kuwa na siku hii, tunasheherekea utaifa wetu kwasababu tunatoka mataifa mbalimbali.” Mill...