Skip to main content

Posts

Showing posts from April 7, 2018

NFRA YAJIPANGA UZINDUZI WA UJENZI WA MAGHALA NA VIHENGE VYA KISASA

Kaimu Afisa Mtendaji mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye kikao cha kazi na wakuu wa idara, vitengo na wafanyakazi wote wa NFRA Mkao makuu Mjini Dodoma, Leo 6 Aprili 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-NFRA Wakuu wa idara, vitengo na wafanyakazi wote wa NFRA Mkao makuu Mjini Dodoma wakifatilia kwa umakini kikao cha kazi kilichoongozwa na Kaimu Afisa Mtendaji mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba, Leo 6 Aprili 2018. Kutoka kushoto ni Meneja Rasilimali watu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Fredy Mbonde, Afisa Ugavi NFRA Magreth Salia Kavishe, na Mhandisi Imani Nzobonaliba ambaye ni Mhadisi Mwandamizi NFRA wakifatilia kwa umakini kikao cha kazi kilichofanyika katika Ofisi za NFRA Mtaa wa Kizota Mjini Dodoma, Leo 6 Aprili 2018 Mhandisi Imani Nzobonaliba ambaye ni Mhadisi Mwandamizi NFRA na Mratibu wa Mradi wa kuongeza uwezo wa uhifadhi wa...

“FEDHA ZA UPANUZI WA VITUO VYA AFYA ZIFANYE ZAIDI...”, RC GALLAWA

Grace Gwamagobe-Songwe Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa amesema atahakikisha anasimamia kwa ukaribu fedha zilizotolewa na serikali Mkoani hapa kwa ajili ya upanuzi wa vituo vya afya ili zifanye kazi zaidi ya ile iliyopangwa awali kutokana na kuongezeka kwa nguvu za wananchi. Gallawa ameyasema hayo mapema jana wakati wa ziara yake Wilaya ya Mbozi alipokagua maendeleo ya upanuzi wa vituo vya afya vya Isansa kilichopokea milioni 500 na kituo cha Afya cha Iyula Kilichopokea milioni 400, kwa ajili ya ujenzi wa maabara, nyumba ya daktari, chumba cha upasuaji, jengo la mama na mtoto na chumba cha kuhifadhia maiti. “Fedha hizi lazima zifanye kazi iliyopangwa vizuri na pia tuongeze kazi nyingine ya ziada kutokana na kuwa tumepata nguvu ya wananchi lakini pia mafundi wetu hawa tunaowatumia ni wazawa na wenyeji wa maeneo ya kwetu kwahiyo gharama zao zitatupa unafuu ambao tunatakiwa kuutumia kuongeza kazi nyingine”, amesema Gallawa. Mkuu wa Mkoa wa Songwe Chiku Gallawa ak...