MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amewataka wapiga kura wa kata ya Kitwiru, Mjini Iringa kupeleka ujumbe wa hali ngumu ya maisha kwa Rais Dk John Magufuli kwa kumchagua mgombea wa chama chake kuwa diwani wa kata hiyo. “Wakati wananchi wakilalamika vyuma vimekaza, watu hawana hela mifukoni, manunuzi yanapungua na baadhi ya biashara ndogo, za kati na za wawezekazaji wakubwa zikifungwa, kuna baadhi ya madiwani wa upinzani wananuliwa kwa kati ya Sh Milioni 2 na Milioni 5 halafu hela za kodi zinazolipwa na watanzania masikini zinatumika kuitisha chaguzi ndogo kwa gharama kubwa,” alisema. Mbowe alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekuwa ikitumia hadi Sh Milioni 200 kugharamia uchaguzi wa kata moja ambayo diwani aliyekuwepo ananunuliwa kwa Sh Milioni 5. Akizungumzia hali ya maisha ya mtanzania kwasasa Mbowe aliwauliza mamia ya wanachi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni uliomnadi...