Skip to main content

Posts

Showing posts from August 25, 2010

OFISI YA TLP MJINI IRINGA YAPIGWA KUFULI

Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya Uchaguzi Mkuu kufanyika Oktoba mwaka huu, Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Mjini Iringa kimefukuzwa na kutolea vyombo vya nje na Majembe Auction Mart-vijana wa kazi leo baada ya kushindwa lipa kodi pango la ofisi yao ya Shilingi milioni 2,483,624.64 wanalodaiwa na shirika NSSF leo. TLP walipanga katika jengo la NSSF lakini walikuwa hawajalipa kodi ya panga kwa mwaka miwili na hivyo vyombo vyao kuchuliwa na Majembe ilikufidia deni na hatimaye kupiga kufuli ofisi hiyo.

TIMU YA POLISI IRINGA YA AFRICAN LYON 1-0

Timu ya Polisi Mkoa wa Iringa wenye jezi za bluu wakicheza mechi ya kirafiki na Timu African Lyon ambapo timu ya Polisi Iringa iliibuka na ushindi wa bao 1-0 uliyofanyika katika Uwanja wa Samora mjini Iringa leo. Goli hilo lilifangwa na Mshambuliaji na Maiko Mamba wenye jezi nambari 10 mgongoni baada ya kupata pasi kutoka kwa midfielder Bunda Odeni katika dakika 10 kipindi cha kwanza. Bw. Aristos Nakitas Katibu wa C hama cha Soka Morogoro kisalimiana na wachezaji wa timu ya African Lyon  wenye jezi ya orange kabla ya kuanza kwa mechi ya kirafiki leo mjini Iringa. Timu ya Polisi Iringa na picha pamoja na Timu ya Lyon wenye jezi ya rangi ya machungwa. Timu ya Polisi ikipiga picha ya pamoja na viongozi wake wa kwanza kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Timu hiyo  Mohamed Semunya.

MBUNGE WA MUFINDI KASKAZINI ATINGA KORTINI TENA LEO

KESI ya kutoa hongo katika mchakato wa kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) inayomkabili aliyekuwa Mbunge wa Mufindi Kaskazini na Waziri katika serikali za awamu zote nne, Joseph Mungai imetajwa tena leo (Agosti 25) katika Mahakama ya Mkoa wa Iringa. Mungai (66) pamoja na makada wengine wawili ambao ni Katibu wa Umoja wa vijana wa CCM wa Wilaya ya Mufindi, Fidel Cholela (39) na Moses Masasi wanakabiliwa na mashtaka 15 ya rushwa kinyume na sheria ya kuzuia na kupamna na rushwa ya mwaka 2007 na sheria ya gharama za uchaguzi ya mwaka 2010 . Watuhumiwa hao kwa pamoja, kwa mara ya kwanza walipandishwa kizimbani Agosti 11, mwaka huu na kusomewa mashitaka hayo ambayo pia waliyakana. Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkoa, Marry Senapee, ambapo upande wa mashitaka uliokuwa ukiongozwa na Prisca Mpeka kutoka Takukuru, uliomba tarehe nyingine ya shauri hilo kwa ajili ya kusoma maelezo ya awali yanayoweza kuruhusu kuanza kusikiliza kesi hiyo. Hata hivyo, Wakili anayewatet...