Skip to main content

Posts

Showing posts from February 22, 2026

Baraza la Madiwani Mafinga Lapitisha Bajeti ya Sh38.6 Bilioni kwa 2026/27

Mafinga. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Mafinga limepitisha rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Sh38,651,155,000, katika kikao kilichofanyika Februari 21, 2026, kikilenga kuimarisha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo ya mji huo. Akiwasilisha rasimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Afisa Mipango na Uratibu wa Mji, Peter Ngusa, alisema halmashauri imejipanga kukusanya na kutumia fedha hizo katika utekelezaji wa majukumu ya msingi, miradi ya maendeleo na kuboresha ustawi wa wananchi. Alifafanua kuwa kati ya fedha hizo, Sh8,844,800,000 zinatarajiwa kukusanywa kutoka mapato ya ndani, Sh942,454,000 ni ruzuku ya matumizi mengineyo (OC), Sh23,376,336,000 ni ruzuku ya mishahara, na Sh5,487,565,000 ni ruzuku kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Kwa mujibu wa mpango huo, vipaumbele vilivyowekwa ni pamoja na kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, kununua maeneo kwa ajili ya uwekezaji, kuendeleza shamba la parachichi la Makal...

Lutevele, Ng’umbi Wawahamasisha Vijana Stendi Ya Mafinga, Wachangia Sh700,000 Kuimarisha Umoja

Na Mwandishi Wetu Mafinga. Mbunge wa Mafinga Mjini, Dickson Lutevele maarufu kama ‘Villa’, akishirikiana na Mbunge wa Viti Maalumu – Mwakilishi wa Vijana, Jasmin N'gumbi, amewataka vijana wanaofanya shughuli katika Stendi ya Mabasi Mafinga kuimarisha umoja wao ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo. Akizungumza na vijana hao, Lutevele alisema mshikamano na umoja ni nguzo muhimu itakayowawezesha kupata mikopo, mafunzo pamoja na mitaji kupitia mipango ya uwezeshaji wa vijana. “Serikali imeweka mazingira rafiki kwa vijana kujikwamua kiuchumi, lakini ni lazima muwe na umoja imara na vikundi vinavyotambulika rasmi ili iwe rahisi kuwafikia na kuwasaidia,” alisema Lutevele. Kwa upande wake, N’gumbi aliwahimiza vijana hao kufanya kazi kwa nidhamu na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuharibu taswira ya eneo la stendi, akisisitiza kuwa umoja wao utawapa sauti ya pamoja katika kudai na kupata haki zao. Katika kuonesha dhamira ...