Skip to main content

Posts

Showing posts from October 15, 2015

BREAKING NEWS....Mwenyekiti wa NLD, Emmanuel Makaidi afariki dunia

Dk. Emmanuel Makaidi enzi za uhai wake. MWENYEKITI Mwenza wa Ukawa na Mwenyekiti wa chama cha NLD, Emmanuel Makaidi amefariki dunia leo mchana kwa shinikizo la damu akiwa Hospitali ya Nyangao mkoani Lindi. Wasifu wake Alizaliwa Aprili 10, 1941 huko wilayani Masasi mkoani Mtwara. Alianza elimu katika Shule ya Msingi Namalenga wilayani Masasi kati ya mwaka 1948 – 1952, mwaka 1953 – 1954 alisoma katika Shule ya Kati (Middle school) iitwayo Luatala hukohuko Masasi. Baadaye alijiunga na Shule ya Sekondari ya Chuo cha Mtakatifu Joseph na kusoma kidato cha kwanza hadi cha nne kati ya mwaka 1953 hadi 1956. Makaidi alisoma darasa la 13 na 14 (kidato cha tano na sita) katika Shule ya Sekondari Luhule, Uganda kati ya mwaka 1957 – 1958. Baada ya hapo alielekea Afrika Kusini na kujiunga na Chuo Kikuu cha Witwatersrand na kuhitimu Shahada ya Uendeshaji na Usimamizi kati ya mwaka 1958 – 1960. Baada ya kuhitimu vizuri pale Witts, aliendelea kupata ufadhili wa masomo ...

AMKA NA SIMBAYA BLOG NA MAGAZETI LEO IJUMAA

MNUSO WA BIRTHDAY YA MIAKA 70 YA UMOJA WA MATAIFA WAFANA JIJINI DAR #UN70

Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez akipokea wageni nyumbani kwake kwenye mnuso wa birthday ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa jijini Dar.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog ). Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (katikati) akimtambulisha mmoja wa wageni waalikwa kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo (kulia). Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) nchini, Joyce Mends-Cole (kulia) akifurahi jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kushoto) wakati wa zoezi la kupokea wageni waalikwa kwenye mnuso wa birthday ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa Tanzania. Katikati ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la UNESCO Tanzania, Zulmira Rodrigues. Wageni mbalimbali wakiendelea kuwasili na kupoke...