Skip to main content

Posts

Showing posts from September 12, 2025

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NCHINI AWASILI MKOANI IRINGA

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Jenerali Jacob John Mkunda, amewasili mkoani Iringa leo kwa ziara ya kikazi.   Katika ziara hiyo, Jenerali Mkunda amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Komredi Kheri James, pamoja na wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Mkoa ambapo walijadiliana masuala mbalimbali yanayohusu usalama na ulinzi wa wananchi.

CHIEF OF DEFENCE FORCES ARRIVES IN IRINGA REGION

The Chief of Defence Forces of the Tanzania People’s Defence Force (TPDF), General Jacob John Mkunda, has today arrived in Iringa Region for an official working visit. During his visit, General Mkunda held talks with the Iringa Regional Commissioner, Comrade Kheri James, alongside members of the Regional Security Committee, where they discussed various matters related to the safety and security of the public.  

TRA YAZINDUA DAWATI MAALUM LA UWEZESHAJI BIASHARA IRINGA

  Katika jitihada za kuboresha mazingira ya biashara na kuhamasisha ulipaji kodi kwa hiari, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Iringa imezindua rasmi Dawati Maalum la Uwezeshaji Biashara. Hatua hii ni sehemu ya mkakati mpana wa kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi. Akizungumza wakati wa uzinduzi uliofanyika katika viwanja vya Garden, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mnamo 9 Septemba 2025, Meneja wa TRA mkoa wa Iringa, Bw. Peter Jackson, alisema dawati hilo litatoa huduma mbalimbali ikiwemo elimu ya kodi, ushauri wa kisheria pamoja na msaada katika kutatua changamoto zinazowakabili wafanyabiashara katika ngazi zote. “Dawati hili siyo tu sehemu ya kupata taarifa, bali ni jukwaa la mazungumzo ya moja kwa moja kati ya wafanyabiashara na TRA. Lengo letu ni kukuza uelewa wa pande zote na kuendeleza utamaduni wa ulipaji kodi kwa hiari,” alieleza Jackson. Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Bw. Benjamin Sitta, aliwahimiza wafanyabiashara kulitumia vyema dawati hilo, ...