Skip to main content

Posts

Showing posts from October 11, 2017

WAAJIRI WA WATOTO WAFANYAKAZI WA NYUMBANI JIJINI MWANZA WALAUMIWA

Mkufunzi wa mafunzo kwa watoto wafanyakazi wa nyumbani katika Kata ya Buhingwa Jijini Mwanza, akifafanua jambo wakati wa mafunzo hayo hii leo. Mafunzo hayo yafanyika kwenye ukumbi kwa kanisa la AICT Buhingwa kuanzia jana na yatafikia tamati kesho Oktoba 12,2017. Na George Binagi-GB Pazzo Baadhi ya waajiri wa watoto wafanyakazi wa nyumbani jijini Mwanza wameelezwa kuwa kikwazo cha kuwaruhusu watoto hao kupata elimu ya utambuzi yanayotolewa na shirika la WoteSawa. Mratibu wa shirika hilo linalotetea haki na maslahi kwa watoto wafanyakazi wa nyumbani, Cecilia Nyangasi ameyasema hayo hii leo wakati wa mafunzo kwa watoto wafanyakazi katika Kata ya Buhongwa jijini hapa. “Waajiri wamekuwa ni changamoto kubwa kwa sababu wengi wao wanadhani kwamba tunakuja kuwapotosha watoto wao”. Alisema Nyangasi na kubainisha kwamba shirika la WoteSawa linatoa elimu ya kuwajengea uwezo wa kutambua haki zao kisheria, wajibu wao kazini pamoja na elimu ya afya ya uzazi ili...

LHRC YAPINGA ADHABU YA KIFO

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeitaka serikali kubadilisha sharia, kuondoa adhabu ya kifo kwa kuweka adhabu mbadala kwenye makosa ya jinai na wafungwa waliopo katika vifungo vya muda mrefu gerezani. Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na waandishi wa habari juu ya kupinga adhabu ya kifo leo jijini Dar es Salaam. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na Mtandao wa Matukio360, amesema kuwa kituo hicho kinaungana na Mtandao wa Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani katika maadhimisho ya 15 siku ya kupinga adhabu ya kifo. Henga amesema adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili ambayo inakinzana na misingi ya utu na haki za binadamu kama ilivyoainishwa katika mikataba mbalimbali ya kimataifa. “Adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili isiyo ya staha, inayotweza utu wa binadamu, inafanya serikali ionekane pia kama mhalifu kwa kuua, tuitake serikali ibadilishe sharia na k...

WANA GDSS WAFANYA UCHAMBUZI NA KUANGALIA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI KATIKA BAJETI YA TAIFA

Washiriki wa semina za jinsia na maendeleo (GDSS) wamekutana jumaatano hii lengo likiwa ni kujadili ushirikishwaji wa moja kwa moja wa wananchi katika upangaji wa bajeti kuu ya taifa. Mlaghbishi wa semina ya GDSS wiki hii Bw. Hancy Orote akitoa ufafanuzi juu ya jambo fulani katika semina iliyofanyika mapema wiki hii makao makuu ya TGNP Mtandao Mabibo Dar es salaam. Akiongoza semina hiyo mwanaharakati kutoka GDSS Bw. Ance Obote alisema dhumuni la kukutana mahali hapo ni wanaharakati kubadilishana uwezo kuhusu ufahamu, ushiriki na jinsi gani wanatoa elimu hiyo kwa wananchi kuhakikisha wanaitumia haki yao ya msingi ya kushiriki katika bajeti. Muwezeshaji huyo amesema kuwa wananchi huusika sehemu kuu mbili ambazo ni kwenye kupanga vipaumbele na ufuatiliaji(utekelezaji) lakini wananchi hawapewi nafasi ya kupanga vipaumbele na kinachofanyika ni diwani anakutana na mtendaji wa kata na kupanga kipi kianze kama kipaumbele na kipi kiwe cha mwisho. Mshiriki wa semina za GD...

WAZIRI MWIJAGE AMJIBU DANGOTE...

SERIKALI kupitia kwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage imekanusha madai yaliyotolewa na Aliko Dangote kuwa, sera za serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt Magufuli zinatishia wawekezaji. Akizungumza jana, Waziri Mwijage amesema kuwa sera za uwekezaji ziko wazi na zina lenga kuhakikisha kuwa, serikali pia inanufaika na rasilimali za nchi. Dangote ambaye ni tajiri namba moja Afrika alinukuliwa akisema kuwa, serikali imeweka sera ambazo zinaifanya imiliki asilimia kubwa ya hisa kwenye mali. "Wanawatisha wawekezaji wengi, na kuwatisha wawekezaji sio kitu kizuri kufanya," alisema Dangote katika mkutano wa Afrika uliofanyika jijini London. Dangote ni miongoni mwa wawekezaji Tanzania ambapo anamiliki kiwanda cha saruji chenye thamani ya Tsh 1.3 trilioni katika Mkoa wa Mtwara. Waziri Mwijage alisema kuwa, wawekezaji katika Sekta ya Uchimbaji wanatakiwa kutoa umiliki wa asiliimia 16 kwa serikali ili kuhakikisha kuwa nchi ...

Wasanii wa Tigo Fiesta watembelea Duka la Tigo Iringa

Msanii Madee akisalimiana na mtoa huduma wa Tigo mara baada ya kuwasili dukani hapo. Wasanii wakisalimiana na watoa huduma wa Tigo Iringa. Wasanii wakiwa kwenye picha ya pamoja duka la Tigo Iringa