Baadhi ya majeruhi wa ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Shabiby na lori la mizigo lililokuwa likisafirisha vinywaji baridi aina ya Pepsi wameeleza kwa masikitiko namna walivyookoka katika tukio hilo lililotokea katika Kijiji cha Tanangozi, Kata ya Mseke, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Ajali hiyo ilitokea baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso, na kusababisha vifo na majeraha kwa abiria kadhaa. Mwandishi wa The Guardian alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na kuzungumza na baadhi ya majeruhi wanaoendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wengi wakiwa tayari wameruhusiwa baada ya hali zao kuimarika. Mmoja wa majeruhi hao, Juma Shaban, mwalimu wa Songwe Tech Secondary School mkoani Songwe, alisema wakati ajali inatokea alikuwa amelala usingizi ndani ya basi akiwa safarini kuelekea Mbeya. “Nilikuwa nimelala kabisa. Ghafla nikasikia kelele za watu wakivunja vioo vya basi ili kuwaokoa abiria. Nilipojitambua nilikuwa navuja damu nyingi na mguu wangu ulikuwa umevunj...
Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TFS na Meneja wa Rasilimali Watu, Bahati Mtomaye alisema kuwa matumizi sahihi ya Mifugo pamoja na kuzingatia maadili ni nguzo muhimu katika kuboresha utendaji wa taasisi na kujenga imani kwa umma Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TFS na Meneja wa Rasilimali Watu, Bahati Mtomaye alisema kuwa matumizi sahihi ya Mifugo pamoja na kuzingatia maadili ni nguzo muhimu katika kuboresha utendaji wa taasisi na kujenga imani kwa umma. Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya matumizi sahihi ya mifumo katika utendaji. Na Fredy Mgunda, Mufindi WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeanza kuonyesha msimamo mkali katika vita dhidi ya rushwa na ukiukwaji wa maadili kwa kuwataka watumishi wake kuzingatia kikamilifu nidhamu ya kazi na matumizi sahihi ya mifumo ya kiutumishi, hatua inayolenga kuongeza uwajibikaji na ufanisi katika utendaji. Msisitizo huo umetolewa katika siku ya pili ya semina ya mapambano dhidi ya rushwa na maadili kwa maafisa na askari wa Shamba la Miti Sao Hill,...