Skip to main content

Posts

Showing posts from August 7, 2015

CHIKU ABWAO NA MWANAHAMISI MUYINGA WASHINDA KURA MAONI ACT WAZALENDO...!

Mgombea Daudi Masasi aliyepata kura 21, agoma kusani matokeo kutokana na alichodai kuwa hajaridhishwa na  mchako. Mgombea Chiku Abwao  aliyepata kura 25, akisani matokeo.  ALIYEKUWA Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chiku Abwao ameshinda kura za maoni za chama cha ACT Wazalendo ikiwa ni siku chache toka ajiunge na chama hicho. Ushindi mwembamba wa kura 25 alizopata dhidi ya mgombea mwenzake Daudi Masasi aliyepata kura 21, umemuweka katika nafasi ya kuteuliwa na chama chake hicho kipya kuwania ubunge wa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa baadaye mwaka huu. Kabla ya kujiunga na ACT Wazalendo, Abwao alipania kugombea ubunge katika jimbo la Isimani kupitia Chadema, lakini kwa kile alichoita hila zilizokuwa zikifanywa dhidi yake na mbunge wa jimbo la Iringa Mjini anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa ndoto yake hiyo imekoma. Kabla ya kushinda kura hizo za maoni Abwao alise...

MWAKALEBELA: WANASIASA TUSIINGILIE KAZI ZA KITAALAMU

Mkuu wa Wilaya wa Wanging’ombe, mkoani Njombe Frederick Mwakalebela akifungua warsha ya kujifunza kwa pamoja juu ya utekelezaji wa mpango wa usimamizi na matumizi endelevu ya rasilimaliza maji (UMURAME) iliyoandaliwa na Bodi ya Maji Bonde la Rufiji kwa kushirikiana na Shirika la WWF Tanzania iliyofanyika mkoani Njombe jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) Mkuu wa Wilaya wa Wanging’ombe, mkoani Njombe Frederick Mwakalebela (wa tatu kushoto walioketi) akiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kufungua warsha ya kujifunza kwa pamoja juu ya utekelezaji wa mpango wa usimamizi na matumizi endelevu ya rasilimaliza maji (UMURAME) iliyoandaliwa na Bodi ya Maji Bonde la Rufiji kwa kushirikiana na Shirika la WWF Tanzania iliyofanyika mkoani Njombe jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) Mkuu wa Wilaya wa Wanging’ombe, Frederick Mwakalebela ametoa wito kwa wanasiasa kutoingilia kazi ya wataalam katika mipango yao ya ugawaji vibali vya matumizi ya rasilimali za maji katika wi...

MAZUA SMART SHAVERS YAJA NA MUONEKANO MPYA

Muonekano mpya wa nje wa MAZUA Smart Shavers iliyopo maeneo ya KIBAMBA HOSPITAL (stand ya mabasi). Haya sasa kwa wakazi wa UBUNGO,,,,,,,KIMARA,,,,,,,MBEZI LUIS,,,,,,,,KIBAMBA,,,,,,,,,,KIBAHA na maeneo mengine yoote ya jiji la Dar es Salaam....sasa hakuna haja tena ya kuhangaika na foleni kwenda mjini kunyolewa ama KUPAMBA MAHARUSI wa kiume, Sasa mmesogezewa huduma nyumbani......ni MAZUA SMART SHAVERS✔️ iliyokuja na muonekano mpya inapatikana eneo la KIBAMBA HOSPITAL (stand ya mabasi) ukiwa unatoka mjini ni mkono wako wa kushoto na kwa wanaotoka Kibaha ni mkono wa kulia ng'ambo ya barabara. MAZUA SMART SHAVERS✔️ndio wadau wa kwanza kwa Dar es salaam na Tanzania nzima kwa ujumla, kuwekeza mamilioni ya pesa kwa ajili ya kujali afya na vichwa vya wateja wao. Tembelea MAZUA SMART SHAVERS upate huduma tofauti kwa bei ya kawaida kabisa kutoka kwa vijana nadhifu pamoja na warembo maridadi.....Pia kuna chumba cha VIP kwa wateja. WOTE MNAKARIBISHWA KUPATA HUDUMA ILIYO...