Skip to main content

Posts

Showing posts from October 7, 2014

NAPE: JIMBO LA IRINGA MJINI MPANGAJI WAKE KODI YAKE IMEKWISHA

Kamanda wa UVCCM mkoa  wa Iringa Bw  Salim Asas  akisalimiana na katibu wa itikadi na uenezi Taifa  Nape Nnauye  leo  Vijana  wa CCM  wakijiandaa kumvisha skafu katibu mkuu wa CCM taifa Bw Kinana  leo baada ya  kuwasili  Iringa kwa ziara ya  siku 6  Kinana  akivishwa  skafu   Mbunge wa  jimbo la Isimani  Wiliam Lukuvi ambae ni waziri wa nchi ofisi ya  waziri mkuu  sera na uratibu wa bunge  kulia akisalimiana na katibu mkuu wa CCM  Abdulrahman  Kinana lea  baada ya  kuanza  ziara yake  wilaya ya Iringa  Mbunge wa  jimbo la Kilolo na Prof Peter Msolla  kulia akisalimiana na Kinana  Kinana  akisalimiana na viongozi wa CCM wilaya ya Iringa  Kamanda wa UVCCM mkoa  wa Iringa Bw  Salim Asas  akisalimiana na katibu wa itikadi na uenezi Taifa  Nape Nnauye  jana.

KINANA AKUNWA NA UTENDAJI KAZI WA MBUNGE WA KALENGA

Katibu  mkuu  wa CCM Bw kinana  kushoto  akishiriki kuvua  samaki  Kalenga na  mwenyekiti wa CCM mkoa  wa Iringa Jesca Msambatavangu   Kinana  akitazama  bwawa la  samaki na kuvua  samaki Chifu  wa  wahehe   wa pili  kulia  akiwa na wasaidizi  wake  huku  kiti cha kinana  kikiwa  tupu 

WAZUIA MAZISHI YA BIBI YAO

Stori: Victor Bariety, Sengerema WAJUKUU wa marehemu Sabina Ngalu (77) wameibua kutuko makaburini kufuatia kuzama ndani ya kaburi la marehemu huyo na kugoma kutoka wakidai kwamba mpaka walipwe shilingi laki moja (100,000), Uwazi lina mkanda mzima. Wajukuu wa bibi huyo wakiwa kaburini. Tukio hilo la aina yake lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita katika Kitongoji cha Nyamwanza Kata ya Sima wilayani Sengerema mkoani Mwanza muda mfupi baada ya mwili wa marehemu kuwasili eneo la mazishi kwenye shamba lake ukitokea Kanisa la Roman Katoliki Parokia ya Yesu Kristo Mfalme la mjini Sengerema. Sababu za wajukuu hao kung’ang’ania ndani ya kaburi hilo walitaka wapewe ng’ombe mmoja au pesa hizo taslimu kwa mjibu wa mila na desturi za kabila la Kisukuma jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya wanandugu waliodai mila hizo zilipitwa na wakati. Kufuatia wajukuu hao kuendelea kugomea ndani ya kaburi, kaka wa marehemu, Enosi Ngalu alikwenda  kukata fimbo na kuwashukia kisha kuwacharaza...

MAGAZETI LEO JUMANNE

MWANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI AUAWA KISHA KUPORWA PIKIPIKI

Kamanda wa Polisi mkoani Iringa (RPC),Ramadhani Mungi Na Friday Simbaya, Iringa  Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Lugalo ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kichwani na watu wasiofahamika kisha kupora pikipiki yake ambayo haijafahamika namba za usajili.