MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Iringa, ambaye pia ni diwani kata ya Isakalilo, Alex Kimbe (Chadema) pichani kesho saa 5 asubuhi ataongea na waandishi wa habari ofisini kwake, juu ya mustakabali ya Manispaa ya 2015-2020. Diwani wa kata ya Isakalilo, Alex Kimbe (Chadema) jana alichaguliwa kwa kura 21 kuwa Meya wa Manispaa ya Iringa. Kuchaguliwa kwa Kimbe kumemaliza mvutano wa ndani kwa ndani uliokikumba chama hicho wakati kikiwa katika mchakato wa kumpata mgombea wa nafasi hiyo na kumaliza historia enzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoa Meya kila baada ya Uchaguzi Mkuu. Katika kinyang’anyiro hicho ambacho CCM walikuwa wasindikizaji kwasababu ya kuwa na idadi ndogo ya madiwani; mgombea wake Bashir Mtove alijipatia kura 6. Mtove aliwania nafasi hiyo iliyoachwa wazi na aliyekuwa Meya wa miaka mingi wa manispaa hiyo, Amani Mwamwindi ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu, alishinda kwa kura chache kiti cha udiwani wa kata ya Mlandege dhidi ya mgombea wa C...