Skip to main content

Posts

Showing posts from November 6, 2010

HONGERA DK SHEIN NA MAALIM SEIF

SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WATU WENYE ULEMAVU TANZANIA (SHIVYAWATA), ambalo ni muungano wa vyama tisa vikuu vya kitaifa vya watu wenye ulemavu tofauti nchini vinampongeza Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Serikali ya Baraza La Mapinduzi Zanzibar 2010 – 2015. Halikadhalika muungano huo wa vyama vinampongeza Maalim Seif Sharif Hamad pamoja na chama chake Chama cha Wananchi (CUF) kwa kuchaguliwa kuwa mshindi wa pili kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), lakini pia kwa busara aliyoionyesha ya ukomavu wa kisiasa kwa kukubali matokeo na kuepusha vurugu ambazo zingeweza kutokea kama angeamua vinginevyo. Kukubali kwake matokeo si kwamba kumeepusha vurugu tu, bali pia kumeepusha maafa na ongezeko kubwa la watu wenye ulemavu, lakini pia ifahamike kuwa machafuko yoyote yatokeapo waathirika na wahanga wakuu wanakuwa ni watu wenye ulemavu, akinamama, wazee na watoto, hivyo basi Mwenyekiti –SHIVYAWATA Lupi Maswanya Mwaisak...
KIKUNDI cha Sanaa cha ‘Imarisha Vijana Ongeza Ajira’ (IVA) kilichopo Kata ya Ludewa, wilayani Ludewa Mkoa wa Iringa kikicheza ngoma za asili za Lugambusi na Kihoda hivi karibuni. Kikundi hicho pia kinaelimisha jamii juu ya Ukimwi, Mazingira pamoja na kufanya shughuli za maonesho katika sherehe za kitaifa nchini. (PICHA: FRIDAY SIMBAYA)

AFYA

Afya ni mtaji, fundi rangi alikutwa akikwangua rangi katika kuta za Jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF-AKIBA HOUSE) Mkoani Iringa linalofanyiwa ukarabati, huku vumbi likimtimkia bila kifaa cha kuzuwia vumbi bila kujali madhara yanayoweza kumpata. (PICHA: FRIDAY SIMBAYA)