Na Vicky Macha, Iringa. MADEREVA wanatakiwa kuzingatia alama za barabarani ili kukabiliana na ajali za mara kwa mara hasa zinazojitokeza katika barabara kuu ya Tanzania na Zambia (TANZAM). Rai hiyo ilitolewa jana na Mkandarasi wa Mradi wa ujenzi wa barabara kutoka makao makuu (Tanroads) Kenfas Mahenge wakati wa makabidhiano rasmi ya barabara hiyo na makandarasi wa kampuni ya Aarsleff- Interbeton Denmark mara baada ya kumalizika kwa ujenzi wa barabara hiyo mwishoni mwa wiki. Mahenge alisema hali ya nchi ilivyo ambayo ni ya milima, miteremko na kona nyingi hasa katika maeneo ya hifadhi ya wanyamaMikumi ni lazima kila dereva kuzingatia alama hizo pindi apitapo katika barabara hiyo kwani kumekuwa na ongezeko la ajali zinazoendelea kuwatafuna wananchi hasa abiria. Alisema kwa kuliona hilo walilazimika kumtaka mkadarasi kuweka kila eneo alama ikiwemo matuta, lakini kumeoneka madereva kuendesha magari kwa uzoefu mba...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.