WAKATI wananchi wanajiandaa kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imewahukumu Majuto Kisumbe (22)na Zawadi Mdegela (33) kulipa faini ya laki moja au kwenda jela mwaka mmoja baada ya kukiri kosa la kujiandikisha zaidi ya mara moja kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura . Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Andrew Peter Scout alisema Kisumbe na Mdegela wamehukumiwa kulipa faini au kenda jela mwaka moja kwa kosa la kujiandisha mara mbili kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura (BVR) kinyume na Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010. Alisema kuwa katika nyakati tofauti Kisumbe, mkazi wa Mahenga wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa na Zawadi Mdegela wa Ifunda wilayani Iringa walijiandikisha mara mbili katika BVR katika vituo viwili tofauti. Hakimu Mkazi Andrew Peter Scout alisema Kisumbe alitenda kosa hilo tarehe 04 Aprili mwaka huu katika Kijiji cha Mahenge, Wilaya ya Kilolo. Alisema kuwa mtuhumiwa Kisumbe al...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.